Breaking News

Your Ad Spot

May 19, 2011

MZEE RUKSA AUNGURUMA NEW YORK

*Asema ruksa kuwekeza  na kufanya
 biashara Tanzania
*Lakini ruksa hiyo ni kwa biashara halali
Na Mwandishi Maalum,
Rais Mstaafu wa awamu ya pili Mzee Ali
Hassan Mwinyi akizungumza na wanachama
na wajumbe bodi ya taasisi ya The Turkish-American
Business Improvement and Development Council
( TABID) ya Jijini New York, Marekani.
piicha zaid mwisho wa stori

New York
Rais  mstaafu wa awamu ya pili Mhe. Ali Hassan Mwinyi amewataka wafanyabishara wa kimarekani  na kituruki kuja  kuwekeza nchini Tanzania na kwamba kwa kufanya hivyo hawatajutia mitaji yao.
Akizungumza na   wanachama na wajumbe wa bodi   ya  taasisi isiyo ya kiserikali ijulikanayo kama  Turkish-American business improvement  and development council ( TABID) ya jijini New York, Marekani.Rais Mwinyi  alitumia fursa hiyo kuitangaza Tanzania kwa kuelezea fursa na maeneo ya uwekezaji yaliyopo nchini.
Katika  mazungumo yake na wanachama hao,Rais huyo mstaafu  ambaye amefuatana na mkewe Mama Sitti Mwinyi, amesema,  zipo fursa nyingi na maeneo mbalimbali ya uwekezaji ilimradi uwekezaji huo uwe ni halali. “Njooni Tanzania,  njooni mjionee nini  Tanzania inaweza kuwapa, kuna msemo usemao kuona ni kuamini, licha ya  haya ninayowaeleza njooni mjionee wenyewe. Kuna kila fursa ya kuwekeza, ili mradi biashara hiyo iwe halali, nina wahakikishieni hamtajutia uamuzi wenu wala mitaji yenu”.Akasisitiza.
Akasema kwa kuanzia  wafanyabiashara na wawekezaji  hao  wanaweza kuja kushiriki maonesho ya Kimataifa  ya Biashara ambayo hufanyika kila tarehe saba ya kila mwezi wa saba maarufu kama Saba-Saba
“Ninawakaribisha  mje na mshiriki kwenye maonesho haya, hili ni eneo moja la kujionea fursa za uwekezaji na biashara, mtakutana  na kubadilishana mawazo na wafanyabiashara wa ndani na nje, njooni tunaihitaji mitaji yenu na teknolijia zenu” akasihi Rais Mstaafu.
Akasema  inasikitisha kuwa licha ya Tanzania na  Marekani kuwa na uhusiano na ushirikiano mzuri lakini kumekuwapo na pengo kubwa katika ushirikiano wa kibiashara na uwekezaji.
Amesema kasoro hiyo inatokana na matumizi ya watu wa kati na mawakala ambao kwa namna moja ama nyingine wameshindwa kuendeleza na kuvutia  ushirikiano wa kibiashara na uwekezaji kati ya nchi hizo  mbili.
Baadhi ya maeneo ambayo Rais Mwinyi ameyataja kuwa yanahitaji  uwekezaji ni pamoja na kilimo.
Akizungumzia eneo hilo, rais mstafu amesema Tanzania inayo hazina kubwa ya  ekari 88 milioni ambazo zinafaa kwa kilimo lakini kati ya hizo ni   ekari milioni  13 tu ambazo zinatumika kikamilifu
Kuhusu  kilimo cha umwagiliaji amesema Tanzania  imebarikiwa  kuwa na mito na maziwa ambayo maji yake yanafaa kwa kilimo cha umwagiliaji, huku kukiwa na zaidi ya ekari milioni moja ambazo zinafaa kwa kilimo cha umwagiliaji  ingawa ni  ekari 160.000 ambazo zinatumia kilimo hicho
Akasema Tanzania hivi sasa imejiwekea  na inatekeleza sera na mipango inayolenga kuleta mageuzi ya kilimo kupitia mpango wake  ujulikanao kama Kilimo Kwanza.
Hata hivyo amesisitiza kuwa pamoja na mipango mizuri ya kukifanyia mageuzi makubwa kilimo, mageuzi hayo yanaweza yasifanikiwe sana  kama  hapatakuwapo na uwekezaji  katika kilimo cha kisasa na kinachotumia  teknolijia za kisasa.
“ Hili ni eneo ambalo wamerakani na waturuki mnayo fursa kubwa ya kuwekeza, tunahitaji zana na teknolojia za kisasa, tunahitaji  viwanda vya  zana za kilimo na usindikaji za mazao yatokanayo na kilimo, tunauhitaji utaalamu wenu njooni tunayo ardhi kubwa  na ya kumtosha kila mmoja wetu” akasititiza Rais Mstaafu.
Aidha ameyataja maeneo mengine ambayo yanafaa kwa uwekezani kuwa ni katika eneo la viwanda vikubwa na vya kati,  ukanda maalum wauwekezaji maarufu kama  EPZ na  SEZ,madini, utalii, ujenzi wa miundombinu na uhamishaji wa teknolojia za kisasa na mitaji.
Akielezea zaidi ni kwa nini anawashawishi wamarekani na waturiki kuwekeza nchini Tanzania, Rais Mwinyi anasema  Tanzania  kupitia serikali yake imeweka sera, sheria na mazingira mazuri ya  kufanya biashara zikiwamo sheria za kumlida mwekezaji, mali zake na mitaji yake bila ya kubagua kama mwekezaji huyo ni wa ndani au kutoka nje.
Aidha kama hiyo  haitoshi anasema Tanzania  ni  kitovu kikuu cha uwekezaji kwa kuwa inapakana na nchi kadhaa  ambazo   wawekezaji  watanufaika kwa kuuza bidhaa zao katika nchi hizo.
Kwa mfano anasema kuwa Tanzania ni mwanchama wa Jumuia ya Afrika Mashariki(EAC) na  Jumuia ya Maendeleo ya Nchi za Kusini (SADC)  huku kukiwa na jumla  yatu milioni 300 ambao ni mtaji tosha kwa biashara.
Na kubwa zaidi anasema Tanzania ni nchi ya amani, utulivu na salama.
Rais Mstafu  kwa kushirikiana na Balozi wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Ombeni Sefue  pia alijibu maswali  mbalimbali kutoka  kwa watu waliokuwa wakimsikiliza.
Rais Mstaafu  Ali Hassan Mwinyi akionesha zawadi aliyokabidhiwa na wenyeji wake
Baadhi wa wanachama na wajumbe wa Bodi ya TABID wakimsikiliza Rais Mstaafu Mwinyi hayupo pichani. Aliyekaa mbele mstari wa kwanza kutoka kushoto
ni  Mke wa Rais Mama Sitti Mwinyi
Balozi wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Mhe Ombeni Sefue, Rais Mstaafu Ali Hassan
Mwinyi na  Rais wa  TABID Bw. Gokhan Ozkok wakijiandaa kujibu maswali mara baada ya Rais Mstaafu kumaliza mazungumzo yake ya kuitangaza Tanzania na vivutio vyake  katika maeneo ya biashara na uwekezaji. 

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages