Breaking News

Your Ad Spot

Sep 22, 2011

MUKAMA ATEMA CHECHE IGUNGA

Katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mukama akizungumza na waandishi wa habari leo,katika Ofisi ya CCM wilaya ya Igunga mkoani Tabora, kueleza tathmini na mwenendo wa kampeni za CCM za uchaguzi mdogo jimbo la Igunga. Kulia ni Katibu wa Halmsahauri Kuu ya Taifa ya CCM, Oganaizesheni Asha Abdallah Juma.
      Akizungumzia tathmini alisema kampeni zinaenda vizuri na CCM inaonyesha kuwa inaungwa mkono na wananchi wengi wa Igunga na hivyo inatarajia ushindi wa uhakika uchaguzi utakapofanyika Oktoba 2, mwaka huu baada ya kampeni.
     Pia ametumia nafasi hiyo kuvitaka vyombo vya habari kuandika habari zao kulingana na taaluma inavyowataka badala ya kuandika uongo kwa maslahi ya vyama wanavyopendelea au wanavypenda wao iwe.
    Mukama aamelaani na kutangaza hadharani kwamba CHADEMA wameleta makomandoo jimbo ni na kuwasambaza katika kata kadhaa kwa lengo la kutosha wananchi na kufanya fujo katika kampeni zinazoendelea na wakati wa uchaguzi.
      Akitaka kata walimo makomandoo hao, Mukama amesema pia wengi wao wamepata mafunzo nchi za nje. Hata hivyo alikataa kuwataja majina ili kuiwezesha serikali kufanyia kazi kikamilifu taarifa ambavyo CCM imeripoti kuhusu hali hiyo.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages