Breaking News

Your Ad Spot

Apr 29, 2012

SIMBA LEO KAZI MOJA TU, USHINDI TAIFA


Kikosi cha Simba

Baada ya kusubiriwa kwa hamu mechi muhimu ya Kimataifa kati ya Simba na Al Ahly Shandy kutoka Sudan katika mchezo wa hatua ya 16 bora ya michuano ya Kombe la Shirikisho (CAF), leo ndio leo, kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
   Kutokana na umuhimu uliopo ambao si kwa Simba tu ila kwa Watanzania wote, Uwanja wa Taifa unatarajiwa kufurika mashabiki kibao wa soka na bila shaka wale wenye tofauti za kiitikadi katika soka wataachana nazo kwanza na kuungana na wenzao kulishangilia Simba kuipa moyo ili iweze kuibuka na ushindi.
 Viingilio katika mechi hiyo ambavyo tiketi zake zilianza kuuzwa tangu juzi mpangilio wake ni hivi, Viti vya bluu na kijani itakuwa Sh. 5,000, Rangi ya Chungwa Sh, 10,000, VIP C 15,000, VIP B 20,000 na VIP A 30,000

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages