Breaking News

Your Ad Spot

May 3, 2012

NGORONGORO HEROES UGENINI KHOTOUM, MECHI YAO NA WENYEJI KUINGIA BURE


Ngorongoro Heroes

Katika hali inayoonyesha Sudan kuwa na kiu ya kuibuka na ushindi, imeamua watazamaji kuingia bure katika mechi ya timu ya soka ya Tanzania ya Vijana chini ya miaka 20, Ngorongoro Heroes na timu yao ya vijana, itakayopigwa Jumamosi hii, kuanzia saa 2 usiku kwenye Uwanja wa Khartoum.

Ngongoro Heroes waliwasili mjini Khatoum, jana saa 4.00 usiku, tofauti na muda waliotarajiwa wa  saa 2.10 usiku,  lakini haikuwezekana kutokana na ndege  kuchelewa kuondoka kwa saa moja na  nusu kutokana na hali ya hewa kuwa mbaya katika Uwanja wa  Ndege wa Kimataifa wa Jomo  Kenyatta (JKIA) kutokana na mvua kubwa.

Baada ya kuwasili Taka Hotel  ambapo imefikia, Ngorongoro Heroes  ilifanya mazoezi ya saa moja kuanzia  saa 4.30 usiku kwenye Uwanja wa  Khartoum ambao ndiyo utakaotumika  katika mechi dhidi ya Sudan.

Katika mechi ya awali  Ngorongoro Heroes ilishinda mchezo  wa kwanza mabao 3-1 kwenye  Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Hoteli ya Taka ndipo pia timu ya El  Merreikh ya hapa Sudan imeweka  kambi yake kujiandaa kwa mechi ya  marudiano ya Ligi ya Mabingwa Afrika  dhidi ya TP Mazembe ya Jamhuri ya  Kidemokrasi ya Congo (DRC). El  Merreikh ililala mabao 2-0 katika  mechi ya kwanza iliyochezwa jijini  Lubumbashi.

Kwa mujibu wa kocha Kim Poulsen,  wachezaji wote wako katika hali nzuri  na kikosi kitakachoanza kwenye mechi  hiyo kitajulikana kesho (Ijumaa)  baada ya mazoezi ya mwisho  yatakayofanyika saa 2 usiku kwenye  Uwanja wa Khartoum.

Wachezaji walioko kwenye kikosi cha  Ngorongoro Heroes ni Aishi Manula,  Ramadhan Singano, Hassan Dilunga,  Frank Damayo, Frank Sekule, Issa  Rashid, Hassan Ramadhan, Saleh  Malande, Said Zege, Emily Mugeta,  Jerome Lambele, Samir Ruhava,  Simon Msuva, Thomas Ulimwengu,  Atupele Green, Dizana Yarouk, Jamal  Mroki na nahodha Omega Seme.

Mwamuzi Aden Abdi Djamal wa  Djibouti ndiye atakayechezesha mechi  hiyo. Djamal atasaidiwa na Wadjibouti  wenzake Egueh Yacin Hassan,  Bogoreh Salime Fahan na Aden Ali  Farah. Waamuzi hao watawasili kesho  (Ijumaa) saa 8 mchana kwa ndege ya  Ethiopian Airlines wakati Kamishna wa  mechi hiyo Patrick Naggi kutoka Kenya  atawasili leo (Alhamisi) saa 2.10 usiku  kwa ndege ya Kenya Airways.

Iwapo Ngorongoro Heroes itafanikiwa  kuitoa Sudan itacheza mechi ya raundi  ya pili dhidi ya Nigeria.

Mechi ya  kwanza itchezwa Julai 28 mwaka huu  jijini Dar es Salaam wakati ya  marudiano itakuwa kati ya Agosti 10  na 12 mwaka huu.

Ikifanikiwa kuitoa Nigeria, Ngorongoro  Heroes itacheza mechi ya raundi ya  tatu na mshindi kati ya Afrika Kusini  na Congo Brazzaville.

Mechi ya  kwanza itakuwa ugenini kati ya  Septemba 21 na 23 mwaka huu wakati  ya marudiano itakuwa nyumbani  Oktoba 6 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages