Breaking News

Your Ad Spot

Jun 12, 2012

MAMBO YA MISS UTALII TANZANIA

Ikiwa ni wiki moja tu tangu Bodi ya Taifa ya Mashindano ya Miss Utalii Tanzania kutangaza , kuigawa mikoa yote ya Tanzania bara na visiwani katika kanda maalumu za Mashindano hayo ya Miss Utalii Tanzania .
       Mvutano mkubwa ulijitokeza mingoni mwa wadau wa Mashindano hayo, kwa upande wa kanda za Miss Utalii Tanzania – Kanda ya Ziwa na Miss Utalii Tanzania – Kanda ya Magharibi, ambapo kila upande ulikuwa ukidai kuongezewa mikoa katika kanda yake, huku mkoa wa Kagera wakitaka kuwa kanda ya Ziwa na Mkoa wa Shinyanga wakitaka kuwa kanda ya Magharibi , huku wakitaka mkoa wa Mara upelekwe kanda ya Ziwa sambamba na Mkoa wa Mwanza.
     Chanzo cha mvutano huo imebainika ni kugombea nafasi za kuwa wenyeji wa Fainali za Kanda za Mashindano haya, wakati Shinyanga wakiamini kuwa uwepo wao katika kanda moja na Mara na Mwanza
kutawaondolea fulsa ya heshima ya kuwa wenyeji wa Fainali za Miss Utalii Tanzania – Kanda ya Magharibi kama ambavyo Mkoa wa Mara nao wanaamini kuwa kuwepo katika kanda moja na Mikoa ya Kagera na
Shinyanga kutawaomdolea fulsa ya kupewa heshima hiyo kubwa ya kuwa wenyeji wa Fainali za Miss Utalii Tanzania – Kanda ya Magharibi, huku wakitanabaisha kuwa bora wasiwe na Mashindano hayo Mkoani Mara kuliko kuwekwa kanda moja na Mwanza. Inadhaniwa pia kuwa hofu ya mikoa hiyo kuwa kanda moja na mkoa wa Kagera, ni hisia kuwa Kagera inaweza kupendelewa kuwa wenyeji wa Fainali za kanda kwa kuwa waziri wa Maliasili na Utalii ni mmoja wa wabunge wa Mkoa wa Kagera.
      Bodi ya Taifa ya Mashindano ya Miss Utalii Tanzania , imekaa tena na kutafakari na kuzingatia maoni ya wadau mbalimbali wa Utalii,Utamaduni na Mashindano haya, ambapo imeridhia kuwa Mgawanyo wa mikoa na kanda za Mashindano haya ya Miss Utalii Tanzania , unakidhi matakwa ya kukuza na kuyafikisha Mashindano haya kuanzia Ngazi za Vijiji,Majimbo, Wilaya, Mikoa, Taifa na Dunia, aidha Mgawanyo huu umezingatia uwepo wa vivutio vya Utalii, Utamaduni katika maeneo husika na pia gharama za uendeshaji na uandaaji wa kiwango cha kimataifa. Mgawanyo huu ,umezingatia kutoa fulsa kwa kila mkoa kujitangaza
kitalii,kitamaduni na kiuwelezaji kitaifa na kimataifa. Mgawanyo pia unazingatia uungaji mkono na utekelezaji wa vitendo wa sera za taifa za Utalii, Utamaduni, Uwekezaji, Mazingira, Afya, Umasikini, Elimu,
Vijana, Wanawake na watoto kupitia Mashindano haya ya Miss Utalii Tanzania.
    Mgawanyo huu utasadia pia kutekeleza malengo mahususi ya Mashindano haya ikiwemo kuhamasisha na kukuza Utalii wa ndani, kupigavita mila, tamaduni komgwe na potofu na kumfanya kila mtanzania kuwa balozi wa Utalii na utamaduni wa Tanzania ikiwa ni kuunga mkono juhudi za Serikali za kukuza na luifanya Tanzania kuwa miongini mwa nchi zinazoongoza kwa pato la Utalii Duniani, na kufanya kila makao makuu ya wilaya ,mikoa na majiji kuwa na mazingira ya kuvutia watalii wa ndani na nje.
     Mgawanyo huu hauna mahusiano yoyote ya jusiasa wala kabila kwani asasi ya Miss Tourism Tanzania Organisation siyo ya kisiasa, kikabila wala kidini,ambayo ipo ili kutekeleza, kuhamasisha na kutafsiri kwa vitendo sera za taifa za Serikali za Utalii, Utamaduni, uwekezaji, Mazingira, Afya, Elimu n.k.
     Tunafahamu fika kuwa mkakati huu ni pigo na kikwazo kikubwa kwa wasio
yatakia mema Mashindano haya , ukiwemo ule mtandao wa kuchafua,kudhoofisha na kukwamisha jitihada za ustawi wa Mashindanohaya kitaifa na kimataifa. Mgawanyo kamili wa wa kanda na mikoa wa
Mashindano haya ni kama ifuatavyo:

MGAWANYO WA MIKOA NA KANDA ZA MASHINDANO YA
MISS UTALII TANZANIA
Na.    KANDA    MIKOA
    Miss Utalii Tanzania Kanda ya Mashariki    Morogoro, Pwani na Tanga  Miss Utalii Tanzania Kanda ya Magharibi    Kagera, Shinyanga,  Kigoma na Mara   Miss Utalii Tanzania  Kanda ya Ziwa    Mwanza, Geita, Tabora na Shimiyu  Miss Utalii Tanzania Kanda ya Kaskazini    Arusha, Kilimanjaro na Manyara
    Miss Utalii Tanzania Kanda ya Kati    Dodoma, Singida na Morogoro  Miss Utalii Tanzania  Kanda ya
Kusini Nyanda za Juu      Mbeya, Rukwa na Katavi   Miss Utalii Tanzania Kanda ya Kusini    Ruvuma, Iringa na Njombe Miss Utalii Tanzania Vyuo Vikuu  Kanda ya Kati      Dodoma, Tabora, Singida,     Miss Utalii Tanzania Vyuo Vikuu Kanda ya Kusini    Ruvuma, Iringa na Njombe   Miss Utalii Tanzania Vyuo Vikuu
Kanda ya Pwani      Dar es Salaam, Zanzibar, Lindi na Mtwara   Miss Utalii Tanzania Vyuo Vikuu Kanda ya Magharibi    Kagera, Shinyanga,  Kigoma na Mara    Miss Utalii Tanzania Vyuo Vikuu Kanda ya Kusini Nyanda za Juu      Mbeya, Rukwa na Katavi    Miss Utalii Tanzania Vyuo Vikuu Kanda ya Kaskazini    Arusha, Kilimanjaro na Manyara   Miss Utalii Tanzania Vyuo Vikuu Kanda ya Mashariki    Morogoro, Pwani na Tanga    Miss Utalii Tanzania Vyuo Vikuu Kanda ya Ziwa     Mwanza, Geita, Tabora na Shimiyu

Asante,
Miss Utalii Tanzania ni Alama ya Urithi wa Taifa – Utalii ni Maisha,
Utamaduni ni Uhai wa Taifa.

Erasto Gideon Chipungahelo
Rais na Mtendaji Mkuu Miss Tourism Tanzania Organisation

--
Miss Tourism The Symbol Of National Heritage

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages