Breaking News

Your Ad Spot

Oct 23, 2012

UCHAGUZI MKUU UVCCM, MGOMBEA AJITOA WAKATI WA KUOMBA KURA

Lulu akitangaza kujitoa

NA BASHIR NKOROMO, DODOMA
Wakati ilitarajiwa kwamba uchaguzi wa kumpata Mweneyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM (Taifa) ungeweza kutoa ushindani zaidi kutokana na nafasi hiyo kuombwa na wagombea wa jinsia zote, hali ilibadilika ghafla baada ya mgombea pekee mwanamke, Lulu Abdalla Msham kuamua kujiondoa badala ya kuomba kura.

Kufuatia kujiondoa kwake  mwanamke huyo, nafasi hiyo ilibaki ikiwaniwa na madume wawili, 
Msaraka Rashid Simai na Khamis Sadifa Juma wote kutoka zanzibar.

Katika uchaguzi huo uliofanyika baada ya kufunguliwa na Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete, kwenye Ukumbi wa Mwalimu Nyerere mjini Dodoma, nafasi ya Makamu Mwenyekiti wamechuana Ally Salum Hapi, Paul Christian Makonda Mboni Mohamed Mhita.

Nafasi nyingine ni, Halmashauri Kuu ya Taifa Viti sita (Bara) wagombea 40, Viti Vinne (Zanzibar) wagombea 22, Nafasi ya Baraza Kuu la Vijana Taifa Viti vitano Bara wagombea 39 na viti vitano Zanzibar wagombea 14,  Uwakilishi Wazazi Taifa na Jumuia ya Wanawake Tanzania (UWT) wagombea 16 kila nafasi.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages