Breaking News

Your Ad Spot

Dec 22, 2012

WAFANYAKAZI OFISI YA MAKAMU WA RAIS WAPIGWA MSASA KUHUSU BIOTEKNOLOJIA YA KISASA

 Baadhi ya Wafanyakazi wa Ofisi ya Makamu wa Rais wakimsikiliza Katibu Mkuu Bw. Sazi Salula (hayupo pichani) katika semina ya wafanyakazi wa Ofisi hiyo juu ya matumizi salama ya Bioteknojia ya kisasa. Semina hiyo imefanyika leo katika ukumbi wa Karimjee jijiini Dar es Salaam na kuwashirikisha wafanyakazi wa Ofisi ya Makamu wa Rais kutoka Dar es Salaam, Zanzibar na Dodoma.
 Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bw. Sazi Salula (kulia) akifungua rasmi semina ya watumishi wa Ofisi yake kuhusu matumizi salama ya Bioteknolojia ya kisasa. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu Eng. Ngosi Mwihava.
 Mmoja wa wawezeshaji katika semina hiyo Bw. Thomas Bwana - Afisa Kilimo Mwandamizi kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais akiwasilisha mada juu ya Bioteknolojia ya kisasa.
 Mmoja wa wawezeshaji katika semina hiyo Bw. Onesphory Kamukuru - Mhandisi wa Mazingira  kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais akiwasilisha mada juu ya usimamizi wa matumizi salama ya Bioteknolojia ya kisasa.
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Sazi Salula akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Ofisi yake kutoka Ofisi za Dar es Salaam, Dodoma na Zanzibar mara baada ya kufungua semina ya matumizi salama ya Bioteknolojia ya kisasa

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages