Breaking News

Your Ad Spot

Apr 18, 2013

CCM: SARAKASI ZA CHADEMA BUNGENI NI DHIHAKA KWA WANANCHI

NAPE

GAIRO, MOROGORO, Tanzania
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimeeleza kukerwa kwake na matukio ya kejeli matusi na uvunjifu wa amani yanayoanza kushamiri bungeni na kusema kuwa matukio hayo ni dhihaka ya hali ya juu inayofanywa na wabunge dhidi ya wananchi waliowachagua.

Hayo yalisemwa na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye wakati akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Uwanja wa shule ya Msingi, Gairo mkoani hapa, Aprili 18, 2013, ambao mgeni rasmi alikuwa Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana.

" Mambo haya yanayofanywa na wabunge  kama ilivyotokea jana (juzi), ni dhihaka inayofanywa na wabunge kwa wanancjhi waliowachagua. Baadhi ya wabunge wanafanya vituko hivi huku wakiwa wanatambua wazi kwamba heshima waliyopewa ni kwenda bungeni kujadili matatizo ya wananchi ambayo ni mengi kama migogoro ya ardhi. Hili tukio la jana ni  aibu ya mwaka", alisema Nape.

Alisema, muda wanaokuwepo bungeni, wabunge wanapaswa kuutumia wote kwa hekima busara na uwezo wao wote kujadili namna ya kuwezesha Watanzania kufikia maisha bora na siyo kuutumia muda huo kujadili tofauti zao za kisiasa au namna ya kutekeleza malengo yao binafsi ya vyama vyao.

"Hatua hii ya wabunge wa Chadema kuamua kuzusha tafrani na kuvunja kanuni za bunge kwa makusudi ni ya hatari sana, hivyo wananchi wanapswa kujifunza kwamba hawa siyo watu wa kuwapa madaraka. Tazama hivi sasa bungeni wapo wachache sasa wananchi wakihadaika wakawachagua na kuwa wengi bungeni patakuwaje? Hili ni fundisho tosha". alisema Nape.

Alisema, hatua ya Wabunge na viongozi wa Chadema kulijadili suala la Mkurugenzi wa Usalama wa Chama hicho, Wilfred Lwakatare kuhusiana na ugaidi huku wakijua kwamba ni suala ambalo lipo mahakamani, ni la kujaribu kuingilia uhuru wa mahakama kwa makusudi ili ifikie mahala mahakama itupilia mbali kesi hiyo kwa kigezo cha kuinngiliwa uhuru wake.

"Haya ni matumzi mabaya ya bunge ambayo yanasukumwa na viongozi wao ikiwemo kuingilia uhuru wa mahakama, ili hatimaye ionekane uhuru wa mahakama umengiliwa kuhusiana na kesi hiyo na hatimaye itupiliwe mbali. Kila mwenye akili anajua kwamba  huu ni mkakati malum wa Chadema", alisema Nape

Mbali na kulizungumzia bungeni suala ya Lwakatare, Chadema wamekuwa wakilisema pia mitaani, akitoa mfano hatua ya hivi karibu ya Mbunge wa Singida, Tuntu Lissu kufanya mkutano na waandishi wa habari kuzungumzia suala hilo na kwamba mbali na kutafuta kesi hiyo itupwe pia ni juhudi za Chadema kujaribu kusukuma maamuzi ya mahakama.

"Inashangaza sana,  Lisu badala ya kutoa ushahidi wake mahakamani kuhusu suala hili anakwenda kuzungumza na wandishi wa habari ili hali anafahamu wazi kwamba kesi kuhusiana na suala hilo ipi mahakamani, tafsiri yake ni kwamba ni juhudi za Chadema kujaribu kusukuma maamuzi ya mahakama au kushawishi mahakama kutupilia mbali kesi kwa kigezo kwamna imeingiliwa uhuru wake", alisema na kuongeza:.

"Mbowe pia wakati akizungumza Bungeni alitumia muda mrefu kuzungumzia suala la Lwakatare lililopo mahakamani. leo mahakama ionekane uhuru wake umeingiliwa iitupe kesi, na hata wakati wa kuchangia bajeti ya Utumishi, upande wa Chadema badala ya kuzungumzia sekta ya utumishi wa umma kurasa nne nzima zilihusu mambo ya Lwakatare", huu ni mkakati mbaya sana  unaolenga haki isitendeke kuhusu kesi hiyo.

Akizungumzia hatua ya Mbunge wa Arusha mjini, Godbless Lema kutamka bungeni kwamba Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Kikwete na Chama Chake  cha CCM ndiyo chanzo cha udini, aling'aka kwamba ni kauli inayotia shaka uelewa wa mambo wa mbunge huyo.

"Nina mashaka kama Lema ni mzima kiakili, CCM italetaje udini wakati ndiyo imeleta umoja na mshikamano kwa makabila zaidi ya 24 ya Tanzania kiasi kwamba amani na utulivu vimeshamiri? Yaani CCM ihangaike kujenga mshikamano halafu hiyo hiyo ione kicefuchefu kuilinda na kuanza kuihujumu? huu ni upuuzi wa hali ya juu sana", alisema Nape.

Nape alisema, vituko vyote vinavyoendelezwa na Chadema Bungeni na kwingineko ni dalili tosha kwamba wanaendelea kutekeleza ahadi waliyotangaza siku nyingi kwamba nchi haitatawalika.

Mkutano huo ulifanyika ikiwa ni sehemu ya ziara ya Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana inayoendelea mkoani Morogoro, ambapo pamoja na Nape, Kinana anafuatana na Katibu wa NEC, Oganaizesheni Mohamed Seif Khatib. Ni ziara ya kukagua uhai wa Chama na utekelezaji wa ilani ya CCM mkoani humo.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages