Breaking News

Your Ad Spot

Sep 13, 2013

BALOZI MPYA WA ITALIA ARIPOTI KWA RAIS KIKWETE

IKUKLU, Dar es Salaam
RAIS  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amepokea hati za utambulisho za Balozi mpya wa Italia katika Tanzania Dk. Luigi Scotto (kulia, akimkabidhi hati hiyo Rais Kikwete).
     Balozi huyo alikabidhi hati zake, kwa Rais Jakaya Kikwete, katika hafla maalum iliyofanyika leo, Ikulu jijini Dar es Salaam.

      Katika mazungumzo bada ya kukabidhi hati, Rais Kikwete amemtaka Balozi huyo kusaidia kuzishawishi kampuni zaidi za Italia kuja kuwekeza Tanzania na kuboresha mahusiano ya kiuchumi wa baina ya   nchi hizo mbili.

    “Tumekuwa na makampuni makubwa ya Italia yaliyopata kuwekeza katika uchumi wa Tanzania ikiwa ni pamoja na Agip na Incar lakini bado tunahitaji uwekezaji zaidi ili tuweze kuimarisha zaidi uchumi wetu,” Rais Kikwete alimwambia Dkt. Scotto.

     Aidha, Rais Kikwete ameishukuru Italia kwa misaada ambayo nchi hiyo imekuwa inatoa kuchangia maendeleo ya Tanzania ikiwamo kugharimia ujenzi wa Barabara ya Dar es Salaam Bagamoyo.

      Naye Balozi huyo mpya kwa upande wake amesema kuwa amefurahi  kuteuliwa kuwa Balozi katika Tanzania.

     “Ndoto yangu kubwa tokea nikiwa mtoto ilikuwa ni kufanya kazi katika nchi iliyomtoa Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere” alisema Balozi Scotto.

       Balozi huyo alipowasili katika viwaja vya Ikulu alipokewa na wenyeji wake na nyimbo za mataifa hayo ziliimbwa zikiongozwa na bendi maalumu iliyoandaliwa kwa ajili ya mapokezi ya balozi.

      Balozi Dkt. Scotto anachukua nafasi ya mtangulizi wake nchini Perluigi Velardi aliyemaliza muda wake wa kulitumikia taifa lake nchini.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages