Breaking News

Your Ad Spot

Sep 14, 2013

WANAFUNZI WAWILI WAJERUHIWA NA MLIPUKO MOROGORO

MOROGORO, Tanzania
WANAFUNZI wawili wa kidato cha kwanza katika shule ya sekondari Matombo katika wilaya ya Morogoro wamejeruhiwa baada ya kulipukiwa na kitu kinachodhaniwa kuwa ni bomu.
 
Taarifa ilizopata theNkoromo Blog kutoka Morogoro zimesema  wanafunzi hao ambao walikumbwa na dhahama hiyo  wakati wakitoka shule ni Lucien Juma (14) na Anthonia Charles (15), wakazi wa kijiji cha Konde, Tarafa ya Matombo wilayani Morogoro.

Imeelezwa kwamba wakati wa asubuhi wakienda shule wanafunzi hao njiani  waliona kinachofanana na balbu ya tochi wakakipuuza na kwenda zao, lakini wakati wanarudi wakiwa watano, walikikuta tena kitu hicho, mmoja wao aliyekuwa akila muwa, alikirushia kitu hicho ganda ghafla kikalipuka na kutoa mshindo mkubwa uliosikika hadi maeneo ya mbali.
 
Kaimu kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro John Laswai, alithibitisha kujeruhiwa kwa wanafunzi hao, ambapo majeruhi Anthonia ametibiwa na kuruhusiwa na kwamba polisi wanaendelea na uchunguzi zaidi kubaini kitu kilichowajeruhi wanafunzi hao, ambacho kilitoa mshindo mkubwa na mtawanyiko wa vyuma, kama kilikuwa ni bomu ama vinginevyo.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages