Breaking News

Your Ad Spot

Dec 23, 2013

CHOLAGE AFUNGA SEMINA YA UVCCM MABIBO, AKABIDHIWA PICHA ZA NAPE, DK. FENELLA

 MWENYEKITI wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) Kata ya Mabibo, wilaya ya Kinondoni, Zakaria Kimemeneki (kulia), akikabidhi zawadi ya picha ya Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, kwa Katibu wa Jumuia ya Wazazi mkoa wa Dar es Salaam, Mohamed Cholage, wakati wa kufungwa semina ya Baraza la UVCCM kata hiyo, jana. Picha hiyo imetolewa na UVCCM Mambibo, ili akabidhiwe Nape kutokana na kutambua mchango wake katika kuijenga CCM. Zaidi ya Vijana Wajumbe 30 walishiriki semina hiyo.
 Kisha Mwenyekiti huyo akakabidhi picha ya Kamanda wa UVCCM Kata ya Mabibo, Dk. Fenella Mkandara ili nayo imfikie kwa kushukuru mchango wake kwa uilea jumuia hiyo ya Chama usiku na mchana
 Kisha Mwenyekiti huyo wa UVCCM akamvalisha Cholage kofia maalum ambayo UVCCM hao wanasema, walimuona kwa mara ya Kwanza katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana ameivaa ya aina hiyo baada ya kuteuliwa kushika wadhifa huo mjini Dodoma
 Cholage akitoa kitabu cha Kanuni za UVCCM kwa mmoja wa washiriki wa semina hiyo. Kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Kata ya Mabibo, Bononi Mlowe.
 Wanasemina wakimsikiliza mgeni rasmi
Mgeni rasmi akivishwa skafu Cjolage,  baada ya kuwasili kwenye ukumbi. Alisema hii ilikuwa mara yake ya kwanza kuvishwa skafu!!

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages