Rais
wa Klabu ya Bongo Movie Unity, Steve Mengere "Steve Nyerere" katikati
akiwakabidhi vijana wa Kinondoni Jezi na mipira sita Ikiwa nisehemu yake
ya kujitoa Kwa Jamii kwa kile alichoweza. Steve alisema kuwa yeye
ameweza kutoa kile kidogo alichoweza kuwa nacho na anaamini kuwa Jezi
pamoja na Mipira hiyo Sita itaweza kusaidia kuamsha hali ya michezo kwa
Vijana Hao Wa Kinondoni na kuhaidi pia ataendelea kuwasaidia vijana wa
kitanzania katika michezo pale anapoweza kufanya hivyo. Vijana wa
Kinondoni Wamshukuru pia Kwa kuweza kutoa hata hiko kidogo kwani
wanaamini kutoa ni Moyo na Sio Utajiri.
Kiongozi
wa Vijana wa Kinondoni akipokea Jezi kwa Niaba ya Wenzake kutoka kwa
Rais wa Bongo Movie Unity Steve Nyerere mwishoni mwa wiki
Wakiwa katika Picha ya Pamoja mara baada ya kuwakabidhi Jez na Mipira Sita.
Mwishoni
mwa Wiki Rais wa Bongo Movie Unity, Steve Mengere, "Steve Nyerere"
aliwakabidhi vijana wa Kinondoni Jumla ya Mipira 6 na jozi moja ya Jezi
za mpira wa miguu ikiwa ni sehemu ya kujitoa kwake kwa Jamii
iliyomzunguka.
Steve
alisema kuwa ameweza kutoa kile kidogo alichonacho kwaajili ya kuinua
hali ya michezo kwa vijana hao wa Kinondoni kitu ambacho anaamini kuwa
vijana hao watapa hali ya michezo na kuachana na vitendo viovu katika
Jamii, Vilevile aliongezea kusema kuwa ataendelea na moyo huyo kwa kutoa
japo kile kidogo atakachopata kwaajili ya kuendelea kuwasaidia vijana
wa Kitanzania katika Nyanja mbalimbali kwa kuanza ameanza na vifaa vya
michezo kwa vijana hao wa Kinondoni.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269