Breaking News

Your Ad Spot

May 28, 2014

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU)ilipomfikisha Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Da es Salaam, aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umeme(TANESCO), William Mhando na Mkewe Eva Mhando pamoja na maofisa wengine wa serikali makosa mbalimbali likiwemo kosa la matumizi Mabaya ya Madaraka

William Mhando akiingia katika chumba cha Mahakama.
Aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO, William Mhando (kushoto) akitoka katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam Jana , ambapo alisomewa shitaka la matumizi mabaya ya madaraka
---
Na Happines Katabazi 
 TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), ilimfikisha Katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Da es Salaam jana , aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umeme(TANESCO), William Mhando na Mkewe Eva Mhando pamoja na maofisa wengine wa serikali makosa mbalimbali likiwemo kosa la matumizi Mabaya ya madaraka na kughushi.

Mbali na Mhando na Mkewe ambao wanatetewa na wakili wa kujitegemea Jamhuri Johnson, washitakiwa wengine ni Francis Machalange ambaye ni Mhasibu Mkuu wa Tanesco,Sophia Misidai  ambaye ni Mhasibu Mkuu  na Naftali Kisinga  ambaye ni Ofisa Ugavi wa Shirika Hilo.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages