Viongozi wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) wakiwa
wanaendelea kufanya mikutano ya hadhara nchi nzima kudai Katiba ya
wananchi, bado viongozi hao wanasisitiza kwamba kamwe hawatarudi kwenye
Bunge la Malaamu la Katiba kama njia za kistaarabu za kuwaomba warudi
hazitatumika.
Kabla ya kuanza kuzunguka mikoani, Ukawa walianza
kampeni za kudai Katiba inayotokana na maoni ya wananchi kupitia Bunge
Maalumu la Katiba.
Ukawa wanapinga mchakato huo kutekwa na CCM, kwa
madai kuwa wamekuwa wakitumia wingi wao ndani ya Bunge hilo kuchakachua
maoni yaliyotolewa na wananchi kupitia Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269