Waziri wa Habari Mheshimiwa Dkt.
Fenella Mukangara
---
Waziri wa Habari Mheshimiwa Dkt.
Fenella Mukangara amewatumia salamu za rambirambi waandishi wa habari
kufuatia kifo cha Mpiga picha wa kituo cha television cha Mlimani, Ndugu
Maximilian John kilichotokea alfajiri ya kuamkia Jumamosi wiki
iliyopita.
Dkt. Mukangara amesema amepokea
kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha Bwana Maximilian
kilichotokana na maradhi ya Moyo, Sukari na Shinikizo la damu na
ameongeza kuwa kifo hicho ni pigo na pengo kubwa kwa tasnia ya habari
hapa nchini.
Amesema Bw. Maximilian
atakumbukwa kwa uchapakazi na uhodori wake wa kazi zake uliokuwa
unazingatia weledi wa taaluma ya uandishi wa habari, jambo lililomfanya
awe na marafiki wengi wa tasnia hiyo.
“Nakutumia salamu zangu za
dhati kuomboleza msiba huu mkubwa kwa watumishi wote wa Mlimani TV,
tasnia ya habari na familia yake kwa ujumla, amesema Dkt. Mukangara.
Ameongeza kuwa Bw. Maximilia
atakumbukwa daima na waandishi wa habari na wadau wengine kwa ucheshi
wake,ushirikiano na wenzake wakati wa kutekeleza majukumu ya kitaalum na
ujenzi wa Taifa kupitia Sekta ya habari.
“Ninaungana na waandishi wa
habari na wadau wengine katika kumwomba Mwenyezi Mungu, Mwingi wa
Rehema, aiweke peponi roho ya marehemu. Amen,” amesema Dkt.Mukangara.
Imetolewa na;
IDARA YA HABARI, VIJANA , UTAMADUNI NA MICHEZO
26 Mei, 2014
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269