Breaking News

Your Ad Spot

Jul 11, 2014

DAWASA KULIPA FIDIA YA SH. BILIONI NANE KWA WANANCHI BWAWA LA KIDUNDA


MOROGORO, Tanzania
MAMLAKA ya Maji safi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASA) inatarajiwa kulipa karibu sh. Bilioni 8 kwa wananchi wanaoisho karibu na bwawa la Kidunda, Morogoro.

Mkurugenzi  wa fedha wa  DAWASA Didas Mwilawi alisema hayo leo wakati wa kikao cha watendaji wa Mamlaka hiyo na Halmashauri ya wilaya ya Morogoro.

Amesema fedha hizo zitalipwa kwa utaratibu wa hundi  kwa wananchi wote ambao  tayari walishahakikiwa na kupewa fomu ya  fidia namba 69.

"Fomu hii ilitolewa na maafisa ardhi wakati wa uthamini wa fidia  na inayo kumbukumbu namba, mfidiwa atatakiwa kuonyesha fomu hiyo kama ushahidi" alisema.

Alisema kwa wananchi walioko jirani na bwawa hilo watatakiwa kuhama ndani ya miezi 6 huku wale wale ambao barabara imepita maeneo yao watatakiwa kuondoka ndani ya miezi mitatu kupisha ujezi  huo.

"Ni lazima tuanze kutengeneza barabara inayoanzia Ngerengere hadi katika bwawa hilo alafu ndipo tuanze ujenzi wa bwawa" alisema.

Mbunge wa jimbo la Morogoro  Kusini Inocent Karogeries aliwataka wananchi hao kuhakikisha fedha hizo wanazitumia kujenga makazi bora na sio kuzitumia katika matumizi mengine.

Mwenyekiti wa halimashauri ya wilaya ya Morogoro Kibena Kiongo  aliwataka viongozi kutowalazimisha wananchi hao na kuwachgulia Benk ya kujiunga kwaajili ya zoezi hilo na badala yake wawaache wenyewe wafanye maamuzi.

Naye mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Morogoro Yona Maki alisema tayari viwanja 1000 ( elfu moja vimeshapimwa kwaajili ya  makazi ya wananchi hao.

Alisema watu 2600 ndio wanatakiwa kufidiwa katika zoezi hilo kwa upande wa barabra itakapopita na wale wanaishi jirani na bwawa hilo.

Bwawa la Kidunda linajengwa kwaajili ya kuchukua maji kutoka katika mto Ruvu kwaajili ya   kusaidia kuwa na uhakika wa maji katika kipindi chote cha mwaka.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages