Breaking News

Your Ad Spot

Sep 14, 2014

KINANA APIGA KAZI MKURANGA SIKU YA KWANZA YA ZIARA YAKE MKOANI PWANI

 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akichanaganya udongo huku Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akisubiri kubeba, waliposhiriki kwenye ujenzi maabara ya  shule ya sekondari Mwalusembe, wilayani Mkuranga  mwanzoni mwa ziara katika mkoa wa Pwani, Septemba 13, 2014.
 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akibeba ndoo ya udongo kipeleka eneo la ujenzi, yeye na Kinana waliposhiriki kwenye ujenzi maabara ya  shule ya sekondari Mwalusembe, wilayani Mkuranga mwanzoni mwa ziara katika mkoa wa Pwani, Septemba 13, 2014.
Kinana akishiriki ujenzi shule ya sekondari Mwalusembe wilayani Mkuranga
Wadau wa maendeleo wakishiriki kunyanyua matofali ujenzi maabala shule ya Mwalusembembe, wakati wa ziara hiyo ya Kinana.
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akinyanyua tofali lililovyafuliwa na kijana Amina Ally (kulia), alipokagua ujenzi wa  maabara katika shule ya sekondari Mwalusembe akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa ilani ya CCM na kusikiliza kero za wananchi na njia ya kuzitatua katika mkoa wa Pwani.
 Kinana akihutubia mamia ya wananchi katika mkutano wa hadhara Kimanzichana wilayani Mkuranga mkoa wa Pwani. Kushoto ni Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akifuatilia hali ya mambo.
 Mwenyekiti wa UWT na mbunge viti maalum mkoa wa Pwani, Zainab Vulu akihutubia wananchi katika mkutano wa Kinana uliofanyika viwanja vya CCM, Kimanzichana wilayani Mkuranga mkooa wa Pwani.
 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia katika mkutano wa Kinana uliofanyika septemba 13, 2014, kwenye Viwanja vya Ofisi ya CCM, Kimazinchana wilayani Mkuranga mkoa wa Pwani.
 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia katika mkutano wa Kinana uliofanyika septemba 13, 2014, kwenye Viwanja vya Ofisi ya CCM, Kimazinchana wilayani Mkuranga mkoa wa Pwani.
 Mamia ya wananchi kwenye mkutano wa Kinana Mkuranga
 Wananchi kweneye mkutano wa Kinana Kimanzichana
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akizindua shina la wajasiriamali wakereketwa wa CCM, Kimanzichana. Kulia ni Nape. (Picha zote na Bashir Nkoromo)

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages