Breaking News

Your Ad Spot

Feb 27, 2015

AL SHAIMAR KWEIGYIR AMTEMBELEA MAJERUHI WA TUKIO LA UPORWAJI WA MTOTO MWENYE ULEMAVU WA NGOZI ALBINO (ALBINISM) YOHANA BAHATI


Na Mwandishi Wetu, Mwanza
Mbunge wa kuteuliwa, Al Shaimar Kweigyir,
amtembelea majeruhi wa tukio la uporwaji wa mtoto mwenye ulemavu wa ngozi
albino,Yohana Bahati, aliyetekwa nyara na kukutwa akiwa amekufa.
 
Katika ziaraa hiyo kwenye Hospitali ya Bugando jijini
Mwanza, Mh Shaimar aliongozana pia na Katibu Tawala Msaidizi wa Ofisi ya Mkoa
wa Mwanza, Crencencia Joseph na August Tesha, ambaye ni Meneja wa Bayport
Financial Services mkoani Mwanza.
Wakiwa Hospitali ya Bugando, Mbunge Shaimar na alioambatana
nao alipata fursa ya kuzungumza na wahudumu katika wodi aliyolazwa Ersther
ambaye ni wa Yohana na kumfariji katika kipindi kigumu cha kuuguza majeraha
yake pamoja na kulia msiba wa mwanae.
 
Tukio la utekaji na uporwaji wa watu wenye ulemavu wa ngozi
limezidi kushika kasi, ambapo kumekuwa na malalamiko mengi kutoka kwa wadau,
hususan wale wenye ulemavu wa ngozi wakiamini kuwa serikali imeshindwa
kuwapatia ulinzi wa kutosha.
 
Akiwa jijini Mwanza, Mbunge Shaimar na taasisi ya kifedha ya
Bayport Financial Services watakuwa kwenye safari ya kuelekea wilayani Kwimba
kwa ajili ya kwenda eneo alilokuwa akiishi Ester na watoto wake, hususan wawili
kati ya watano waliobaki wakiwa ni albino.
Mbunge wa kuteuliwa Shaimar Kweigyir katikati akiwa na bibi wa Yohana Bahati (Tabu Maganiko) kulia ambaye ni mlemavu wa ngozi aliyeuawa hivi karibuni mkoani Mwanza, huku mama yake akiachwa na majeraha makubwa wakati wanagombania mtoto katika tukio hilo la kusikitisha. Kushoto kwake ni Mweka Hazina wa Chama Cha Albino Tanzania Abdullah Omari.
Katibu wa Mheshimiwa mbunge, Semeni Kingalu, kulia akipiga picha wakati walipomtembelea majeruhi Ester Maganiko, ambaye mtoto wake Yohana Bahati mwenye ulemavu wa ngozi aliuliwa katika tukio hilo la kusikitisha. Anayefuata ni Muuguzi wa zamu wa Hospitali ya Bugando na Clencencia Joseph, Katibu Tawala Msaidizi Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mwanza.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages