Balozi Seif Iddi: Jukumu kubwa la Vyuo vya Elimu ya Juu nchini ni kutoa taaluma inayolenga kurahisisha utekelezaji wa mipango ya maendeleo ya Taifa
Wahitimu
wa Chuo cha Elimu ya Baishara Pemba wakiandamana kuingia katika uwanja
wa Michezo wa Chuo cha Amali Vitongoji kwa ajili ya Hamafali yao baada
ya kumaliza mafdunzo yao ngazi ya Cheti.
Wahitimu
wa Chuo cha Elimu ya Biashara Pemba wakiwa tayari kuthibitishwa
kukamilisha mafunzo yao na kupewa vyeti vyao kwenye mahafali yao ambapo
mgeni rasmi alikuwa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali
Iddi.
Baadhi
ya wahitimu wa Chuo cha Elimu ya Biashara Pemba wakifuatilia matukio
mbali mbali kwenye mahafali yao iliyofanyika katika viwanja vya Chuo cha
Amali Vitongoji Chake chake Pemba.
Mohammed
Suleiman Khalfan akipokea tuzo na fedha taslim kutoka kwa Balozi Seif
baada ya kuwa Mwanafunzi Bora wa Fani ya Hesabu katika chuo cha Elimu ya
Biashara Pemba.
Balozi
Seif akimzawadia Tuzo na Fedha Taslim Mwanafunzi Bora wa Fani ya
Mawasiliano ya Umma wa Chuo cha Elimu ya Biashara Pemba Nassor Mussa
Khamis kwenye mahafali ya chuo hicho hapo Vitongoji Chake Chake Pemba.
Balozi
Seif akiwa katika picha ya pamoja na Uongozi wa Bodi ya chuo cha elimu
ya Baishara pamoja na Serikali Mkoa wa Kusini pemba mara baada ya
kukamilika kwa mahafali ya kwanza ya chuo hicho. Kulia
ya Balozi Seif ni Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo akiwa pia Mkuu wa
Wilaya ya Mkoani Nd. Hemed Suleiman Abdullah, Mkuu wa Chuo hicho
Abdulwahab Said Abubakari na Mhadhiri wa chuo hicho Moh’d Said. Kushoto
ya Balozi Seif ni Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Mh. Mwanajuja Majid na
Mkuu wa Wilaya ya Chake chake Bibi Hanuna Ibrahim Masoud.
Balozi
Seif akiwa katika Picha ya pamoja na Uongozi na wahadhiri wa chuo cha
elimu ya Biashara Pemba mara baada ya kukamilika kwa mahafali ya kwanza
ya chuo hicho tokea kilipoanzishwa Januari 2014. (Picha zote na Hassan Issa– OMPR – ZNZ)
Na Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
22/2/2015.
MAKAMU
wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alisema kwamba jukumu
kubwa la Vyuo vya Elimu ya juu hapa nchini ni kutoa Taaluma inayolenga
kurahisisha utekelezaji wa mipango ya Maendeleo ya Taifa pamoja na Jamii
kwa ujumla.
Alisema
fikra za kupanua wigo katika kuongeza fani ya teknolojia ni muhimu
zaidi kwa vile itasaidia vijana kuweza kuendana na wakati wa sasa wa
mabadiliko ya Sayansi na teknolojia.
Balozi
Seif alieleza hayo kwenye mahafali ya kwanza ya chuo cha elimu ya
Biashara Pemba yaliyofanyika katika viwanja vya chuo cha Amali kiliopo
Vitongoji Wilaya ya Chake chake Mkoa wa Kusini Pemba.
Alikishauri
chuo hicho kuangalia namna ya kujiunga na Taasisi mbali mbali za
Kimataifa za Elimu ili kujiimarisha zaidi pamoja na kupata fursa za
kubadilishana uzoefu na utaalamu miongoni mwa walimu na wanafunzi.
Balozi
Seif alisema zipo Taasisi nyingi za kielimu Duniani ambazo chuo cha
Elimu ya Biashara Zanzibar kinaweza kushirikiana nazo ili kupiga hatua
za haraka kitaaluma sambamba na kuliongezea Taifa Wataalamu
watakaosaidia taasisi za umma na hata zile Binafsi.
“
Mnaweza kushirikiana na taasisi kama vile Association of Business
Excutives { ABE }, Chartered Institute ofManagement { CIMA } za
Uingereza, Institute of Hospitality { IH } na Association of
Information Technology Professionals { AITP } za Marekabi “.
AlisemaBalozi Seif.
Alihimiza
kwamba ufundishaji wa chuo hicho uelekezwe katika kutoa mchango na rai
tofauti zitazochangia na kurahisisha utekelezaji wa mipango ya Serikali
ikiwemo Dira ya Maendeleo ya 2020,MKUZA 11, pamoja na malengo ya
Milenia.
Makamu
wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliupongeza Uongozi wa chuo cha Elimu ya
Baishara kwa uamuzi wake wa busara wa kuanzisha kwa mara ya kwanza
chuo Binafsi ambacho Makao Makuu yake yapo Pemba wakati jamii imezoea
kuona Matawi ya vyuo vya elimu ya juu ndio yanayofunguliwa Kisiwani
humo.
Alisema
uamuzi wao umepelekea vijana wengi Kisiwani Pemba kupata fursa za
kujiunga na mafunzo ya elimu kwa gharama nafuu tofauti na ile wanayotoa
wakati wanapoamua kufuatia masomo hayo Unguja au Tanzania Bara.
“
Kuna Gharana ya usafiri, chakula na malazi ambazo zinakuwa kubwa na
wengine wanashindwa kuzimudu, lakin i uwepo wa fursa hizo nyumbani
baadhi ya gharama zinapunguwa na nyengine kuondoka kabisa na hivyo
kuwafanya wanafunzi kusoma kwa utulivu “. Alisisitiza Balozi Seif.
Akizungumzia
suala la ajira Balozi Seif alifahamisha kwamba chuo cha elimu ya
Biashara kitakuwa na mchango mkubwa katika Taifa la Tanzania na Jumuiya
ya Afrika Mashariki katika kuzalisha vijana bora kielimu ili kuweza
kukabiliana na ushindani wa ajira ndani ya Jumuiya hiyo.
Alisema
wapo vijana wengi wanaomaliza masomo yao ya sekondari ya vyuo lakini
jamii inapaswa kuamini kwamba Taifa linakabiliwa na tatizo kubwa la soko
la ajira pamoja na soko la biashara linalokabiliwa na changamoto kadhaa
Duniani.
Balozi
Seif alisema ushindani katika soko la ajira utaongezeka kutokana na
Mataifa ya jumuiya ya Afrika Mashariki na soko la pamoja kuelekea kwenye
Umoja wa Kisiasa.
Makamu
wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliwaomba wahitimu wa Chuo cha Elimu ya
Biashara Pemba waendelee kutafuta Taaluma zaidi kwa vile Taifa
linawategemea. Hivyo wanapaswa kujituma zaidi kwa lengo la kuchangia
Maendeleo ya Taifa.
Aliwaasa
wahitimu hao kuelewa kwamba maendeleo ya Taifa yatachangiwa na jitihada
zao kwa vile hakuna Mjomba wa kuja kuwafanyia kazi kuwaletea maendeleo.
Kazi hiyo watalazimika kuitekelza wao wenyewe.
Akisoma
Risala ya Chuo cha elimu ya Biashara Pemba Mkuu wa Cuo hicho Bwana
Abdulwahab Said Aboubakar alisema lengo la kuanzishwa kwa chuo hicho
Januari mwaka 2014 ni kutoa elimu ya Biashara kwa Vijana `ili waweze
kujinasua katika tatizo la ajira.
Alisema
Uongozi wa chuo hicho pia umezingatia katika mambo ya msingi
yaliyotiliwa mkazo zaidi ni pamoja na kutoa ushauri katika fani ya
biashara kwa taasisi na hata jumuiya za kiraia ndani na nje ya nchi.
Mkuu
huyo wa Chuo cha Elimu ya Biashara Pemba aliwashukuru washirika wa chuo
hicho waliochangia kufanikisha uanzishwaji wa chuo hicho ambacho
kitakuwa mkombozi kwa wananchi wa Kisiwa cha Pemba katika masuala ya
Biashara.
Naye
Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo cha Elimu ya Biashara Pemba ambae pia
ni Mkuu wa Wilaya ya Mkoani Nd. Hemed Suleiman Abdulla alisema kulikuwa
na changamoto kubwa sana wakati wa uanzishwaji wa chuo hicho likiwemo
tatizo la ukosefu wa Majengo.
Nd.
Hemed alisema ni faraja iliyoje kwa wananchi wa Kisiwa cha Pemba hasa
Vijana kupata fursa `baada ya kuanzishwa kwa chuo hicho ambayo
itawapunguzia gharama za masomo pamoja na makaazi wakiwa nje ya Pemba.
Makamu
Mwenyekiti huyo wa Bodi ya chuo cha elimu ya Biashara aliwashauri
Viongozi wa Serikali na hata Taasisi za kiraia kuwaruhusu wafanyakazi
wao kupata Taaluma katika chuo hicho ili kuongeza uwezo wa kazi
kitaaluma.
Akimkaribisha
mgeni rasmi katika mahafali hayo ya kwanza ya chuo cha elimu ya
Biashara Pemba Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Mh. Mwanajuma Majid alieleza
kwamba fani ya taaluma ndani ya Kisiwa cha Pemba ilikuwa na ukwasi
Mkubwa.
Mh.
Mwanajuma alisema wananchi wa Pemba hasa Vijana na Wanafunzi sio kwamba
walikuwa hawahitaji kupata elimu ya juu lakini kilichokuwa kikiwakabili
ni changamoto ya gharama za masomo na malazi wakati wakiwa nje ya
Kisiwa hicho.
Mahafali
hayo ya kwanza ya chuo cha elimu ya Biashara Pemba yamejumuisha
Wahitimu 133 wa ngazi ya Cheti katika fani Tano ambazo ni Uhasibu,
Usimamizi wa Biashara, Uongozi wa Rasilmali Watu, Manunuzi na Ugavi
pamoja na Mawasiliano ya Umma.
Balozi
Seif Katika mahafali hayo alipata futrsa ya kutoa tuzo na fedha taslim
kwa wahitimu waliofanya vizuri zaidi kwenye mitihani yao ambao ni
Mohammed Suleiman Khalfan Hesabu, Rashid Ali Rashid Usimamizi wa
Biashara na Rehema Ali Haji Manunuzi na Ugavi, Kassim Juma Rasilmali
Watu pamoja na Nassor Mussa Khamis Mawasiliano ya Umma.
Chuo
cha Elimu ya Biashara Pemba kinachotumia Majengo ya kukodi na kikiwa
katika harakati za kujenga majengo yake ya kudumu hivi sasa kina
Wanafunzi wapatao 175 kati yao asilimia 64.8% ni Wanawake ikiwa juu
zaidi ya Wanafunzi Wanaume ipatayo asilimia 58.2%.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269