Breaking News

Your Ad Spot

Apr 14, 2015

WAMA WAKISHIRIKIANA NA ENGENDER HEALTH WAANDAA SEMINA YA KUZUIA MIMBA ZA UTOTONI KWA WANAFUNZI WA SEKONDARI ZA WILAYA YA TEMEKE.

(PICHA NA JOHN  LUKUWI). 
WA2Baadhi ya wanafunzi na walimu kutoka Shule 11 za Sekondari katika Wilaya ya Temeke wakisikiliza hotuba ya mgeni rasmi, Afisa Elimu-Sekondari wa Wilaya ya Temeke Ndugu Donald Chavila (hayuko pichani) wakati alipokuwa akifungua rasmi semina ya siku tano inayozungumzia uzuiaji wa mimba za utotoni kwa wanafunzi wa Wilaya hiyo tarehe 13.4.2015 kwenye ukumbi wa sherehe wa Kibasila Sekondari. WA4 Afisa Elimu-Sekondari wa Wilaya ya Temeke Bwana Donald Chavila akifungua rasmi semina ya siku 5 ya kuzuia mimba za utotoni kwa wanafunzi wa Shule za Sekondari katika Wilaya ya Temeke. Semina hiyo inaendeshwa na Taasisi ya WAMA, ikishirikiana na Shirika la Engender Health la Marekani na kufadhiliwa na Shirika la Misaada la Serikali ya Marekani,USAID. WA7Baadhi ya wanafunzi na walimu wa Shule za Sekondari kutoka Wilaya ya Temeke wakifuatilia kwa makini hotuba ya Mgeni rasmi, Afisa Elimu-Sekondari wa Wilaya ya Temeke Ndugu Donald Chavila wakati akifungua semina hiyo inayofanyika Kibasila Sekondari.  WA10Baadhi ya wanafunzi kutoka Shule za Sekondari katika Wilaya ya Temeke wakisikiliza kwa maini baadhi ya mada zilizokuwa zikitolewa wakata wa semina ya kuzuia mimba za utotoni kwa wanafunzi wa Sekondari katika wilaya hiyo. Semina hiyo ya siku 5 inafanyika Kibasila Sekondari na ilifunguliwa rasmi tarehe 13.4.2015. WA11Washiriki wa semina wakiwa wamegawanyika katika vikundi mbalimbali ili kujadili mojawapo ya mada iliyokuwa imetolewa na baadaye kila kundi kuwasilisha kwenye semina hiyo. WA13Washiriki wa semina wakiwa wamegawanyika katika vikundi mbalimbali ili kujadili mojawapo ya mada iliyokuwa imetolewa na baadaye kila kundi kuwasilisha kwenye semina hiyo. WA15Mwanafunzi mshiriki wa semina ya kuzuia mimba za utotoni kwa wanafunzi wa shule za sekondari katika Wilaya ya Temeke akiwasilisha majibu ya majadiliano ya kikundi chao katika siku ya kwanza ya semina hiyo.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages