Breaking News

Your Ad Spot

Sep 17, 2015

AMOS MAKALLA AAGA RASMI WIZARA YA MAJI

 Mhe. Amos Makalla akisalimiana na watumishi wa Wizara ya Maji waliompokea mara baada ya kuwasili Wizarani, pamoja na Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu, Gideon Manambo.
Aliyekuwa Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Amos Makalla leo mchana ameaga rasmi watumishi wa Wizara ya Maji na kwenda kuanza majukumu mapya kama Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro.
 Mhe. Makalla ambaye alifika Wizarani hapo, akitokea Ikulu alikoapishwa rasmi na Mhe. Rais, Jakaya Mrisho Kikwete, mara baada ya kuteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro. 
Mhe. Makalla ambaye alikuwa Naibu Waziri wa Maji kwa zaidi ya mwaka mmoja, aliweza kufanya kazi kwa weledi mkubwa licha kuwa mgeni kwenye Sekta hiyo, ambapo aliweza kuzunguka karibu mikoa yote na kutembelea karibu Mamlaka zote za Maji nchini katika kukagua utekelezaji na maendeleo ya miradi ya maji.
 Mhe. Amos Makalla akiwa ofisini kwake, alipofika kuaga Wizara ya Maji.
 Mhe. Amos Makalla akipokea shada la maua kutoka kwa Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala, Beatrice Patrick.
 Mhe. Amos Makalla akizungumza na watumishi wa Wizara ya Maji, wakati akiaga wizarani hapo.
Mhe. Amos Makalla akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi na watumishi wa Wizara ya Maji.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages