Breaking News

Your Ad Spot

Sep 17, 2015

MAMA SAMIA AEKA VILIVYO MIKINDANI NA MAFIA, MIKUTANO YAKE YATIA FORA KWA KUPATA UMATI WA WANANCHI

 Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama samia Suluhu Hassan akihutubia umati wa wananchi katika mkutano wa kampeni, uliofanyika leo katika mji mdogo wa Mikindani mkoani Mtwara.
 Wananchi wakimshangilia Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan katika mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika mji mdogo wa Mikindani mkoani Mtwara
  Wananchi wakimshangilia Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan katika mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika mji mdogo wa Mikindani mkoani Mtwara
 Mgombea Ubunge jimbo la Mtwara mjini, Murji Mohammed akiomba kura baada ya kunadiwa na Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan katika mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika mji mdogo wa Mikindani mkoani Mtwara
 Wasanii wakichangamsha kwa muziki katika mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika mji mdogo wa Mikindani mkoani Mtwara leo
 Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan na Mgombea Ubunge jimbo la Mtwara mjini, Murji Mohammed wakiwapongeza wasanii baada ya kutumbuiza muziki uliosisimua wananchi wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika mji mdogo wa Mikindani mkoani Mtwara
 Kada nguri wa CCM, Kijana Mtera Mwampamba, akimuombea kura Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM, Dk. John Magufuli, katika mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika mji mdogo wa Mikindani mkoani Mtwara
 Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama samia Suluhu Hassan akimpongeza Mtela Mwampamba baada ya kuhutubia katika mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika mji mdogo wa Mikindani mkoani Mtwara
 Vijana wakiwa wameparamia ukuta wa moja ya majengo ya kale, wakati wa mkutano wa kampeni wa Mama Samia uliofanyika katika mji mdogo wa Mikindani mkoani Mtwara leo
 Mwanamuziki wa msanii wa Bongo Movie, Snura akichangamsha mkutano kwa kuimba wimbo wa kuifangilia CCM, wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika mji mdogo wa Mikindani mkoani Mtwara
 Baadhi ya wasanii wa Bongo Movie wakishiriki na wananchi wengine kuselebuka muziki, wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika mji mdogo wa Mikindani mkani Mtwara
 Wananchi wakishangilia wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika mji mdogo wa Mikindani mkoani Mtwara
 Wasanii wa kundi la Hapa ni Kazi Tu, wakionyesha umahiri wao walipotumbuiza katika mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika mji mdogo wa Mikindani mkoani Mtwara
 Mratibu wa 'Mama Sema na Mwanao' Steve Nyerere akiwa na kamarade, Ally Choky, wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika mji mdogo wa Mikindani mkoani Mtwara
 Mgombea Ubunge jimbo la Mtwara Vijijini, Hawa Ghasia akiwa na mtoto aliyepoteana na mama yake, kutokana na wingi wa watu waliofurika wakati wa mkutano wa kampeni za CCM uliofanyika leo katika mji mdogo wa Mikindani mkoani Mtwara
 Mgmbea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akipokea wanachama wapya kutoka vyama vya upinzani, kikiwemo Chadema, katika mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika mji mdogo wa Mikindani mkoani Mtwara
 Mama Samia akiungana na vijana kuishangilia CCM baada ya kuwapokea walipoamua kutangaza kuhamia CCM wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika mji mdogo wa Kimindani mkoani Mtwara leo
"'CCM Hoyeeeee" Kijana Rashid Njechele, akipaza sauti kwa kusema hivyo, baada ya kutangaza kuhamia CCM kutoka CUF, wakati wa mkutano wa kampeni wa Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM Mama Samia (kulia), uliofanyika leo katika mji mdogo wa Mikindani mkoani Mtwara
 Baadhi ya waandishi wa habari na maofisa wa CCM, wakiwa katika ndege, wakati wa safari ya Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM Mama Samia Suluhu Hassan kutoka Mtwara kwenda Kisiwa cha Mafia kufanya mkutano wa kampeni leo.
 Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassani akishuka kwenye Ndege kwenye Uwanja wa Ndege wa Mafia, alipowasili kwa ajili ya kufanya mkutano wa kampeni katika kisiwa hicho leo
 Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Maa Samia Suluhu Hassan akiwa na baadhi ya viongozi waliomlaki kwenye Uwanja wa Ndege wa Mafia, baada ya kuwasili kwa ajili ya kuhutubia mkutano wa kampeni katika kisiwa hicho leo
 Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama samia akisoma baadhi ya mabango yaliyokuwa yamebebwa na wananchi kueleza matumaini yao kwake, wakati wa mapokezi, alipowasili katika Kisiwa cha Mafia kuhutubia mkutano wa kampeni leo. Kushoto ni Mgombea wa Ubunge katika jimbo hilo, Mbarak Dau
 Aliyekuwa Mbunge wa Mafia ambaye pia aliingia katika kinyan'ganyiro cha kuomba ridhaa ya CCm kuwania tena ubunge wa jimbo hilo, Abdulkarim Shah, akimnadi Mgombea wa Ubunge wa jimbo hilo, Mbarak Dau, katika mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika katika Kisiwa hicho cha Mafia
 Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akimpongeza Kada wa CUF, Mohamed Albadawi, baada ya kutangaza kuhamia CCM katika mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika jimbo la Mafia mkoa wa Pwani. Albadawi awali alikuwa Mgombea Ubunge katika jimbo hilo kwa tiketi ya CUF baada ya kuongoza katika kura za maoni, lakini baadaye akaenguliwa na chama hicho na kupachikwa, Shomari Kimbau ambaye alihamia CUF baada ya kushindwa katika kura za maoni za CCM
 Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama samia Suluhu Hassan akihutubia mkutano wa kampeni leo katika Jimbo la mafia mkoa wa Pwani
 Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama samia Suluhu Hassan akimnadi Mgombea Ubunge jimbo la MafiaMbarak Dau katika mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika jimbo hilo mkoa wa Pwani
Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM Mama Samia suluhu (Kushoto), akishiriki kucheza muziki wa taarab uliokuwa ukitumbuizwa na nguli wa muziki huo, Mzee mwishoni mwa mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika jimbo la Mafia mkoa wa Pwani. PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages