Breaking News

Your Ad Spot

Jan 6, 2016

OBAMA ATOKWA NA MACHOZI WAKATI AKITANGAZA NIA YA SERIKALI YAKE KUZUIA MAUAJI YATOKANAYO NA MATUMIZI YA SILAHA ZA MOTO NCHINI HUMO

 RAIS wa Marekani Barack Obama, ametokwa na machozi wakati akitangaza kusudio la mamlaka ya rais (Executive Order), la kudhibiti manunuzi na uuzaji holela wa silaha nchini humo.
Baada ya miaka saba ya kujikokota kwa baraza la kutunga sheria juu ya namna gani watazuia mauaji ya raia wasio na hatia nchini humo. Licha ya ukweli kwamba mauaji yatokanayo na mashambuliji ya silaha za moto yakizidi kupamba moto nchini humo mathalan kwenye miji ya Newtown, Connecticut, San Bernardino, na California.
Akiwa ameambatana na familia za wahanga wa shambulio la Newtown, huku akiwatia moyo waliohudhuria (hadhira), akiwemo Mjumbe mstaafu wa Baraza la  Congress Giffords Giffords, Obama alianza kutoa sauti ya kukwama kwama, na kuwanyooshea kidole wale aliodai wanamtuhumu kudharau misingi ya (second amendment-Mabadiliko ya pili ya katiba ya nchi hiyo) ambayowanaona marufuku mapya ni hatua ya kwanza kuelekea ukwapuzi haki ya kumiliki silaha waliyo nayo Wamarekani chini ya katiba hiyo
“Hao wanaoshawishi umiliki wa silaha, wanaweza kuwawekamateka wajumbe wa baraza la Congress, lakini hawawezi kuwaweka mateka Wamarekani”. Alionya Obama.
Obama aliweka wazi kuwa anaielewa vizuri katiba ya Marekani katika mabadilikohayo ya pili, “Nimesomea masualaya Katiba,” Alisema “Najua kidogo kuhusu hili.”
Sio vema " Uhuru wa mabadiliko ya pili ya Katiba ya Wamarekani ugharimu haki za wote walioangamia kwa kushambuliwa na risasi za moto, haki zao za kushiriki kwenye majumba ya sinema, haki zao za kuabudu kwenye nyumba za Mungu na hakizao za asili za kuishi kwa furaha na amanizimedhulumiwa.


No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages