Breaking News

Your Ad Spot

Feb 17, 2016

JAFARI: MASHAKA YA DUNIA YA SASA NI MATUNDA YA SIASA ZA MAGHARIBI


J'afari: Mashaka ya dunia ya sasa ni matunda ya siasa za Magharibi
Mwakilishi wa kudumu wa Syria katika Umoja wa Mataifa amesema matatizo na mashaka ya sasa ya dunia ni matunda ya siasa za Magharibi hususan Marekani.
Bashar Ja'fari ameliambia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwamba, wawakilishi wa Marekani, Uingereza na Ufaransa wamesahau maafa yaliyosababishwa na siasa za nchi zao katika nchi za Mashariki ya Kati kwa miongo kadhaa iliyopita. Amesema tangu mwanzoni nchi hizo zilianza kutekeleza siasa za kuiunga mkono Israel na kuitayarishia uwanja wa kuzikalia kwa mabavu ardhi za nchi za Kiarabu na zimetumia makumi ya kura ya veto kuukingia kifua utawala huo ghasibu ili watu wa Mashariki ya Kati waendelea kuishi katika mashaka na tabu.
Kuhusu suala la mapambano dhidi ya ugaidi, mwakilishi wa kudunu wa Syria katika Umoja wa Mataifa amesema, njia pekee ya kuaminika katika uwanja huo ni kuunda muungano wa kimataifa kwa mujibu wa sheria za kimataifa na kwa kuzishirikisha nchi zote husika hususan Syria. Amezilaumu baadhi ya nchi kuwa zimekiuka hati ya Umoja wa Mataifa kwa kutuma majeshi katika ardhi ya Syria bila ya idhini ya nchi hiyo na kuficha harakati za magaidi kwa kutumia kisingizio cha kupambana na ugaidi.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages