Breaking News

Your Ad Spot

Feb 5, 2016

KUDHALILISHWA MWANAFUNZI WA KITANZANIA; POLISI WALIAMURU AZIME SIMU YAKE YA MKONONI



NA K-VIS MEDIA NA Mashirika ya Habari

IKIWA ni siku nne tangu msichana wa Kitanzania mwenye miaka 20 anayesoma mjini Bangalore nchini India, kudhalilishwa kwa kuvuliwa nguo na kutembezwa uchi, imeripotiwa Polisi kuwa waliamuriwa na polisi mjini humo kuzima simu zao, Kiongozi wa Wanafunzi Waafrikawanaosoma mjini humo, Bosco Kaweesi amesema.

Kiongozi huyo ambaye pia ni mshauri wa kisgeria wa wanafunzi, ameliambia Jarida la kimtandao Hindustan Time (HT), kuwa polisi walikuwa wanajaribu kuwabana wanafunzi hao ili ukweli na habari kuhusu tukio hilo zisisambae.

Msichana huyo aliyekuwa akisafiri na rafiki zake wengine watatu wa kiume, kwenye garidogo, alikumbana namkasa huo, baada ya kufikaeneo la tukio la ajali iliyosababishwa na raia mmoja wa Sudanaliyemgonga mtu na mkewe na kusababisha kifo cha mwanamke.

Baada ya muda kidogo ndipo Mtanzania huyo na wenzake  w akipita kwenye eneo hilo, walisimamishwa na kuchomolewakutoka ndani ya gari hilo, ambapo wavulana hao walikimbia na kumuacha msichana huyo mikononi mwa genge hilo la watu ambao walimvua nguo na kumtembeza mitaani ikiwa ni pamoja na kumpiga.

Tukio hilo limetafsiriwa na Dunia kuwa ni ubaguzi wa rangi, madai ambayoSerikali ya India pamoja na polisi wamekanusha kuhusisha tukio hilona ubaguzi wa rangi.

Kiongozi wa chama cha wanafunzi wa Tanzania walioko mjini humo, aliyetambuliwa kwa jina moja la Helen, amewalaumu polisi kwa kujaribu kuficha ukweli.
Tayari Waziri wa Mmambo ya Nje, Ushirikiano wa Kikanda, Afrika Mashariki na Kimataifa, Balozi Dkt. Augustine Mahiga, ameliambia Bunge kuwa Serikali inalifuatilia suala hilo kwa karibu sana, na tayari wameambiwa na Serikali ya India kuwa watu watatu wamekamatwa kuhusiana na tukio hilo.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages