Breaking News

Your Ad Spot

Feb 28, 2016

 Askari wa JWTZ, wakiwa na zana zao, sasa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga, atamuomba mwenzake wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, ili "wazee wa kazi" waingie kwenye mapambano  kuwasaka majambazi waliosababisha mauaji ya watu 7 pale Mbagala Rangi-Tatu jijini Dar es Salaam siku ya Ijumaa sa nane mchana baada ya kuvamia na jupora benki ya Access.

NA K-VIS MEDIA
KUFUATIA mauaji ya watu 7 wakiwemo majambazi watatu pale Mbagala Rangi-Tatu, Ijumaa Februari 26, 2016, waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga, amesema atawasiliana na Waziri wa Ulinzi na Jeshi al Kujenga Taifa, ili wanajesi wa JWTZ, wawasaidie polisi kuwasaka majambazi waliotorokea kwenye msitu wa Kongowe.
Waziri ameyasema hay oleo Februari 27, 2016 wakati akizungumzia tukio hilo ambapo majambazi wasio na idadi, wakiwa na silaha nzito nzito walivamia benki ya Acces tawi la Mbagala na kuiba kiasi kikubwa cha fedha ikiwa ni pamoja na kufanya mauaji ya askari polisi mmoja, mlinzi mmoja wa benki hiyo na mfanyakazi.
Pia majambazi hayo yaliua raia wawili kabla ya raia nao kuyaua majambazi matatu huku emngine yakikimbilia kwenye msitu wa Kongowe ulio jirani na eneo la tukio.


 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga
Waziri wa Ulinzi na Jeshio la Kujenga Taifa, Dkt. Hussein Mwinyi

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages