Polisi wa kutuliza ghasia FFU wakiwa
wametinga ndani ya ukumbiwa Karimjee jijini Dar es Salaam jana, tayarikuwatawanya wabunge na madiwani kutoka upinzani baada ya
mkurugenzi wa jiji la Dar es Salaam, kutangaza uchaguzi wa Meya wa jiji
uliopangwa kufanyika jana umeahirishwa tenabaada ya kuwekewa pingamizi
mahakamani.
Na mwandishi wetu
POLISI wa kutuliza ghasia jana walivamiaukumbi wa Karimjee ambapo ukumbi huo ulikuwa umepangwa kufanyika uchaguzi wa Meya wa jiji la Dar es Salaam na kutembeza
virungu kwa wabunge na madiwani wa upinzani wanaounda Vuguvugu la Umoja wa
Katiba ya Wananchi UKAWA.
Vurugu hizo zilizuka baada ya
kutangazwa kuahirishwa kwa uchaguzi huo kwa mara ya nne sasa.
Tukio hilo la aina yake
limetokea muda baada ya Mkurugenzi
wa Jiji la Dar es Salaam kutangaza kuwa uchaguzi huo umeahirishwa akitoa sababu
kuwa uchaguzi umewekewa pingamizi mahakamani, jambo ambalo lilipingwa na wabunge
na madiwani wa UKAWA, wakijenga hoja kuwa bado walikuwa hawajapatiwa barua ya
pingamizi kutoka mahakamani.
Mara baada ya UKAWA kugomea
hoja hiyo ndipo wakafikia hatua ya kutaka kufanya uchaguzi wenyewe huku wakisema akidi ya madiwani
kufanya uchaguzi imetimia na wakaomba waendelee kufanya uchaguzi huo,
Wakati wakijiiandaa kufanya
uchaguzi huo, polisi waaliovaa sare na wale waliovaa kiraia wengine wakiwa na
mabomu ya kutoa machozi, walivamia ukumbini humo na kuamuru waliokuwemo ndani
ya ukumbi huo kutawanyika. Tangazo hilo lilipingwa vikali na wawakilishi hao wa
wananchi na hapo polisi wa kutuliza ghasia hawakuwa na jingine ila kutumia
nguvu kwa kuwaondoa kwa nguvu ukumbini.
Mbunge wa Kibamba John Mnyika akiongoea na simu baada ya kuzuka kwamtafaruku huo |
Polisi wakiwa wamejipanga tayari kuvamia ukumbi huo
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269