Breaking News

Your Ad Spot

Feb 15, 2016

UGANDA YABUNI BASI LINALOTUMIA MWANGA WA JUA, LINAITWA "KAYOOLA" NA LITAZINDULIWA NA RAIS MUSEVENI JUMANNE



UGANDA imetengeneza basi la abiria linalotumia nguvu ya jua kufanya kazi.
Rai wa Uganda Paul Isaac Musasizi ndiye aliyebuni basi hilo na sasa liko tayari kwa safari na litazinduliwa rasmi Jumanne Februari 16, 2016.
Basi hilo litakuwa ni la kwanza la aina yake kubuniwa barani Afrika na kwa mujibu wa taarifa za vyombo vya habari, basi hilo lina uwezo wa kubeba abiria 35 na litakuwa na uwezo wa kutembea
Kijana huyo ambaye ndiye Afisa Mtendaji Mkuu, (CEO) wa kampuni ya Kiira Motors Corporation, amesema kwa vile Uganda wanapata jua siku zote, ndiyo maana aliona abuni basi litakaloendeshwa na nguvu ya jua (Solar Powered electric bus).
Mvumbuzi huyo alisema, basi hilo limepewa jina la kilugha “Kayoola” lina uwezo wa kusafiri maili 50 bila kusimama likitumia betri mbili moja likiwa limeunganishwa na kifyonja mionzi ya jua (Solar Panels), kilichofungwa juu ya basi, na betri nyingine hujichaji kwa safari ndefu hususan wakati wa usiku.
RaisYoweri Museveni anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye uzinduzi huo wa kesho na sasa “Kayoola” ambayo ilifanyiwa majaribio kwenye mitaa ya Kampala na jirani na uwanja wa taifa ndio habari ya mujini.

Wafanyakazi wa kampuni ya Kiira Motors Corporation, wakitazama michoro ya basi hilo wakati wa hatua za mwanzo za kulibuni

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages