Vyama vya upinzani Niger vimepinga matokeo ya awali ya uchaguzi
wa rais ambayo yalionyesha rais wa sasa Mahammadou Issofou akiongoza.
Matokeo ya awali ya maeneo 20 kati ya 308 yalionyesha kuwa Issofou
alipata asilimia 40.18 ya kura zote, ikiwa ni pointi 10 mbele ya
mpinzani wake wa karibu.
"Matokeo haya ni kinyume kabisa cha kile kilichodhihirika katika
masanduku ya kupigia kura," alisema Ahmadou Boubacar Cisse mgombea urais
na msemaji wa muungano wa upinzani.
Kumekuwepo na malalamiko ya wananchi kuhusu uendeshaji mbovu wa
uchaguzi wa Rais uliofanyika siku ya Jumatatu nchini humo. Wapinzani
wanasema kuwa tume ya uchaguzi ya nchi hiyo imevuruga kwa makusudi
uchaguzi huo kwa maslahi ya rais aliyeko madarakani. Rais Mahamadou
Issoufou amegombea kwa mara ya pili katika uchaguzi huo.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269