Breaking News

Your Ad Spot

Feb 24, 2016

AFRIKA KUSINI KUONDOA ASKARI WAKE NCHINI SUDAN

Afrika Kusini kuondoa askari wake nchini Sudan
Afrika Kusini imesema kuwa, ina mpango wa kuondoa askari wake katika jimbo la Darfur la magharibi mwa Sudan.
Ofisi ya Rais Jacob Zuba wa Afrika Kusini imesema leo kuwa, askari wa nchi hiyo wanaofanya kazi chini ya mwavuli wa kikosi cha kulinda amani huko Darfur Sudan wataondolewa.
Ofisi hiyo imeongeza kuwa, askari wa jeshi la taifa la nchi hiyo ambao wamekuweko Darfur tangu mwaka 2008 chini ya mwavuli wa kikosi cha pamoja cha Umoja wa Afrika na Umoja wa Mataifa, watarejea nyumbani tarehe Mosi Aprili mwaka huu, tarehe ambayo ndipo zinapomalizika kazi zao.
Hii ni katika hali ambavyo, hivi karibuni serikali ya Sudan ilikanusha kuwa Umoja wa Afrika umeipa mwaliko rasmi wa kushiriki katika mazungumzo ya amani na waasi.
Tangu mwaka 2003 serikali ya Sudan imekuwa ikipambana na makundi ya waasi katika eneo la Darfur na kwenye mikoa ya Kordofan Kusini na Blue Nile.
Kwa upande wake, ofisi ya kuratibu misaada ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa imesema kuwa, hali ya kibinadamu huko Darfur ni mbaya sana na kwamba kuna uwezekano watu 38 elfu wa Darfur Kaskazini wamekimbia makazi yao.
Takwimu za Umoja wa Mataifa zinaonesha kuwa mgogoro wa Darfur ulioanza mwaka 2003 umeshapelekea zaidi ya watu laki tatu kupoteza maisha yao na milioni mbili na nusu kuwa wakimbizi.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages