NA K-VIS
MEDIA/Mashirika ya habari
Trump,
anayeongoza kwenye kura za maoni kinyang’anyiro cha kumtafuta mgombea wa urais
wa chama cha Republican, amelazimika kujitetea vikali dhidi ya shutuma kutoka
kwa Marco Rubio na Ted Cruz.
Katika
mdahalo huo uliofanyika Detroit, Trump amekiri kwamba amebadilisha msimamo wake
mkali lakini akasema kwamba kuweza kubadilika ni nguvu na si udhaifu.
Baadhi
ya wanachama wakuu wa Republican wanasema Bw Trump hafai na kwamba hawezi
kushinda urais dhidi ya chama cha Democratic.
Mdahalo
huo ulioandaliwa na kituo cha Fox News ulianza kwa Trump kuulizwa kuhusu shutuma za awali kutoka kwa aliyekuwa mgombea
urais wa Marekani kupitia chama cha Republican mwaka 2012 dhidi ya rais wa sasa
Barack Obama, Mitt Romney, aliyesema
mfanyabiashara huyo ni mchokozi, mlafi na aliyejaa chuki na kwa hivyo hfai kuwa
mgombea wa chama hicho na kuwataka Wamarekani hususan wanachama wa Republican
kutomshabikia.
Trump
amempuuzilia mbali Romney na kumtaja kuwa “mgombea aliyefeli”. “Huyu mtu
hujionyesha kuwa ni mnyenyekevu, wakati anagombea alikuwa mnyenyekevu sana
kwangu, na ningeweza kumwambia piga magoti na angepiga, sasa leo anaibuka na
kunishambulia. Alisema Trump wakati akiwa kwenye harakatiza kampeni huko maine.
Akimshambulia
Trump, Mitt Romney alisema, Donald Trump, ameshindwa kwa kila kitu, kashindwa
kusimamia chuo chake kikuu cha Trump University, Na wala sio tajiri kama
anavyodai bali ni utajiri wa kurithi tu sio wa kutafuta mwenyewe, lakini pia
ameshindwa kuendeleza hata kampuni yake ya habari.
Katika
moja ya matukio ya kushangaza, Bw Trump ametetea ukubwa wa mikono yake kisha
akafanya mzaha kuhusu ukubwa wa kiungo chake cha uzazi.
Trump
alitoa utetezi huo baada ya maneno ya mzaha ya mshindani wake, Marco Rubio,
aliyesema, ‘Huyu bwana huniita Marco mdogo, ninakubali yeye ni mrefu kuliko
mimi yeye ana urefu wa inchi 6’2 na ndionashangaa inakuaji mikono ya mtu mwenye
urefu ule ilingane na mtu mwenye urefu wa inchi 5’2. “Alisema Rubio Jumapili
iliyopita huko Virginia. Na kuongeza na mnajua watu husema mtu mwenye mikono
mifupi.” Huwezi kuwaamini.”.
Trump (kulia), akisalimiana na Mitt Romney, wakati huo Romney akiwania urais mwaka 2012
Donald Trump katika moja ya mapozi yake
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269