Breaking News

Your Ad Spot

Mar 20, 2016

KAUNDA: VURUGU KABLA YA UCHAGUZI, ZINACHAFUA USALAMA ZAMBIA

Kaunda: Vurugu kabla ya uchaguzi, zinachafua usalama Zambia
Rais wa Zamani nchini Zambia, Kenneth Kaunda amesema kuwa, vurugu za kisiasa ambazo zimekuwa zikitokea katika kipindi hiki cha kuelekea kwenye uchaguzi wa mwezi Agosti mwaka huu, zinaathiri usalama wa nchi hiyo.
Kaunda aliyeyasema hayo wakati akizungumza katika kikao kilichopewa jina la mhimili wa amani, amewataka wadau wa kisiasa na viongozi wa Tume ya Uchaguzi nchini Zambia kufanya mazungumzo ya kutatua matatizo hayo ya kisiasa. Ameongeza kuwa, hiyo ndio njia pekee itakayosaidia kuimarisha usalama na amani nchini humo. Aidha rais huyo wa zamani wa Zamabia ameyataka makundi tofauti ya kisiasa kuheshimiana, hususan wakati huu wa kuelekea uchaguzi mkuu mwezi Agosti. Migogoro ya kisiasa nchini Zambia imeshika katika katika hali ambayo nchi hiyo inajiandaa kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa rais, bunge na madiwani uliopangwa kufanyika tarehe 11 mwezi Agosti mwaka huu. Kenneth Kaunda alikuwa rais wa Zambia kuanzia mwaka 1964 hadi mwaka 1991.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages