Breaking News

Your Ad Spot

Mar 12, 2016

UCHAGUZI WA MARUDIO ZANZIBAR; KARATASI ZA KUPIGIWA KURA ZAWASILI, ZALINDWA KAMA "LULU"


NA K-VIS MEDIA/Khalfan Said)
KARATASI za kupigia kura kwenye uchaguzi wa marudio visiwani Zanzibar, zimewasili mjini Unguja kutoka zilikotengenezwa nchi Afrika Kusini.
Karatasi hizo ziliwasili Machi 11, 2016 kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Abeid Karume mjini Unguja huku zikilindwa kama “lulu” na polisi waliosheheni silaha.
Karatasi hizo zimehifadhiwa kwenye maghala ya serikali mjini Unguja na zingine zitasafirishwa kwenda kisiwani Pemba tarayi kwa uchaguzi huo wa marudio. Maafisa wa tume ya uchaguzi Zanzibar ZEC wamesema katika taarifa yao iliyotumwa kwa vyombo vya habari ikiambatana na picha za kuwasilikwa karatasi hizo.
Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi Zanzibar, Jecha Salum Jecha tayari amekwisha tangaza kuwa uchaguzi huo utafanyika Machi 20, 2016 na kila kitu kimekamilika, maafisa hao wamesema.
Hata hivyo chama kikuu cha upinzani CUF hakitashiriki uchaguzi huo kwa mujibuwa uamuzi wa Baraza kuu la uongozi la chama hicho.
Hata hivyo maafisa wa ZEC wanasema, hawatambuiuamuzi huo ambao hauko kisheria na ndio maana kwenye karatasi hizi za sa sa za uchaguzi wa marudio, picha za wagombea zikokama zilivyokuwa kwenye ucahaguzi uliopita.









No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages