Breaking News

Your Ad Spot

Apr 27, 2016

WATU 11 WAUAWA KWA KUPIGWA RISASI CAPE VERDE

Watu 11 wauwa kwa kupigwa risasi Cape Verde
Watu 11 wakiwemo askari wanane wameuawa kwa kufyatuliwa risasi viungani mwa mji mkuu wa kisiwa cha Cape Verde.
Paulo Rocha, Waziri wa Utawala wa Ndani wa kisiwa hicho amethibitisha kutokea mauaji hayo ya kutatanisha katika kituo cha mawasiliano katika eneo la misitu la Monte Tchota, yapata kilomita 27 kaskazini mwa mji mkuu, Praia.
Amesema kuwa: "Askari mmoja ambaye alikuwa anaongoza kikosi cha jeshi ametoweka na yumkini ndiye aliyehusika na uhalifu huo."
Rocha ameongeza kuwa, raia wawili wa Uhispania ambao walikuwa wahandisi katika kituo hicho pia wameuawa.
Kadhalika Waziri wa Utawala wa Ndani wa Cape Verde amesema hakuna dalili zozote za kuashiria kuwa mauaji hayo yanahusiana na maswala ya ulanguzi wa mihadarati na kwamba, waliouawa ni watu wenye umri kati ya miaka 20-51.
Kisiwa cha Cape Verde, ambacho kinapatika kaskazini magharibi mwa pwani ya Afrika Magharibi na chenye watu wapatao laki 5, kimekuwa kitovu cha kupitishia dawa za kulevya na haswa cocaine kutoka America ya Latini hadi bara Ulaya.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages