Kaimu
Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) Profesa.
Lawrence Mseru akitoa ufafanuzi kuhusu habari iliyoandikwa na Gazeti la
Mwananchi kuhusu huduma hospitalini hapo leo jijini Dar es Salaam. Kulia
ni Mkurugenzi wa Uuguzi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) Bibi.
Agness Mtawa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Hospitalini hapo Aminiel
Aligaesha.
Picha na: Frank Shija, MAELEZO.
………………………………………………………………………………………………………………
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Profesa Lawrence Mseru ametoa
ufafanuzi kuhusu habari iliyoandikwa katika gazeti la Mwanchi la tarehe
21 Juni 2016 zilizo kuwa zinasema kuwa wagonjwa wa Seli Mundu
wanalipishwa ili kupata huduma ya matibabu yao tofauti ilivyokuwa awali.
Akitoa ufafanuzi huo Profesa
Mseru amesema kuwa kwa habari hizo siyo za kweli kwani wagonjwa wa Seli
Mundu wanatumia utaratibu wa kawaida ambapo mgonjwa utibiwa katika
maeneo wanayotoka na anapaswa kuchangia gharama za matibabu isipokuwa
kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano.
Aliongeza kuwa hapo awali
kulikuwa na mradi wa utafiti wa Seli Mundu ulioenda sambamba na utoaji
wa matibabu kwa wagonjwa waliojumuishwa katika mradi huo uliodumu kwa
muda wa miaka 10 hadi ulipofikia ukomo machi 30 mwaka huu.
Baada ya mradi huo kumalizika
wagonjwa wote walirejea katika maeneo yao ambapo huko wanaendelea na
matibabu kupitia utaratibu wa kawaida huduma za matibabu.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269