Breaking News

Your Ad Spot

Aug 6, 2016

KAMPUNI YA YONO AUCTION MART YAMUUNGA MKONO RAIS MAGUFULI KATIKA JITIHADA ZA KULETA MAENDELEO YA NCHI

 Kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Kampuni ya Udalali ya Yono Auction Mart na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo Bibi. Scholastica Kevela wakiwa wameshika Tuzo na Cheti walivyopewa kutokana na kutoa huduma kwa viwango na ufanisi.Tuzo hiyo inajulikana kwa jina la The Diamond Eye Award for Quality Commitment and Excellence) imetolewa tarehe 25, Julai 2016 Jijini Rome Italia na Rais wa Asasi ya Otherways Management & Consulting ya Paris Ufaransa.
 Mwenyekiti wa Yono Auction Mart & Co Ltd Bw. Stanley Kivela akielezea jambo kuhusu Tuzo ya Almas ya Ubora, Uwajibikaji na Ufanisi (The Diamond Eye Award for Quality Commitment and Excellence) iliyotolewa na Rais wa Asasi ya Otherways Management & Consulting ya Paris Ufaransa ambapo takribani nchi 49 dunia zilishiriki mchakato huo huku Tanzania ikiwakilishwa na taasisi mbili ambazo ni Mamlaka ya Angaa (TCAA) kwa upande wa Serikali  na Yono Auction Mart kwa upande wa Sekta binafsi
 Mkurugenzi Mtendaji wa Yono Auction Mart Bibi. Scholastica Kevela akiwa ameshika Tuzo waliyopewa kutokana na kutoa huduma kwa viwango na ufanisi.Tuzo hiyo inajulikana kwa jina la The Diamond Eye Award for Quality Commitment and Excellence imetolewa tarehe 25, Julai 2016 Jijini Rome Italia na Rais wa Asasi ya Otherways Management & Consulting ya Paris Ufaransa.

Na Frank Shija, MAELEZO.
Serikali ya awamu ya Tano chini ya Rais Magufuli imeendelea  kuungwa mkono na wadau mbalimbali kutokana na jitihada zake za kurejesha heshima na uadilifu miongoni mwa jamii ya Watanzania.
Haya yamebainishwa na Mwenyekiti wa Bodi ya  Kampuni ya Udalali ya Yono Auction Mart & Co Ltd Bw. Stanley J. Kevela aliokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu Tuzo iliyopata leo Jijini Dar es Salaam.
Kevela ameseme kuwa wao binafsi kama kampuni inayoaminiwa na Serikali na taasisi zake wanayosababu ya kuunga jitihada zinazoonyeshwa na Serikali katika kupigania maendeleo ya watu wake kwa kutekeleza majukumu yake kwa uadilifu, ubunifu na ufanisi unaostahili.
“Tunatoa Tuzo hii muhimu kwetu kwa Mhe. Dkt. Magufuli kama ishara ya kuheshimu mchango wake katika kuliletea taifa letu maendeleo  na kuhakikisha mambo yanafanywa kwa ufanisi na  viwango vyenye ubora wa hali ya juu”. Alisema Kavela.
Amesema kuwa tokea Rais Magufuli aingie madarakani mambo mengi yamekuwa yakienda vizuri hivyo ikiwemo suala la ukusanyaji wa Kodi kazi ambayo wamekuwa wakiisaidia Serikali kwa muda mrefu sasa.
Aliongeza kuwa Kampuni yake imekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha inatoa huduma zenye viwango tena kwa uadilifu na uwajibikaji usiotiliwa shaka ndiyo maana wanamuunga mkono Mhe. Rais kwakuwa naye ni muunini wa falsafa ya uwajibikaji, uadilifu na ubunifu.
Aidha Mwenyekiti huyo amesema kuwa katika kuendeleza jitahada za Serikali katika kukuza ajira wameajiri zaidi ya vijana 200 ambao wako mtaani wakifanya kazi ya ukusanyaji wa Kodi kwa niaba ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Yono Auction Marts &Co Ltd Bibi. Scholastica Kevela ametoa rai kwa wadau mbalimbali kuendelea kuiamini Kampuni hiyo kwa kupata huduma zao zikiwemo wakala wa Udalali wa Mahakama na Ukusanyaji wa Mapato ya Serikali kwa niaba ya TRA.
Yono Auction Mart imekuwa ikifanya kazi na Serikali katika Nyanja mbalimba ikiwemo ukusanyaji wa Kodi kwa niaba ya TRA, udalali wa Mahakama, Uuzaji wa viwanja vya Serikali na mambio mengine yanayohusu ukusanyaji wa Kodi za Serikali.
Kampuni ya Yono Auction Marts &Co Ltd ilipata fursa ya kushiriki katika hafla ya ugawaji wa Tuzo za Diamondo Eye kutokana na Ubora, Uwajibikaji na Ufanisi (The Diamond Eye Award for Quality Commitment and Excellence) iliyotolewa tarehe 25 Julai 2016 Jijini Rome, Italy iliyotolewa na Rais wa Asasi ya Otherways Management & Consulting ya Paris Ufaransa ambapo takribani nchi 49 dunia zilishiriki mchakato huo huku Tanzania ikiwakilishwa na taasisi mbili ambazo ni Mamlaka ya Angaa (TCAA) kwa upande wa Serikali  na Yono Auction Mart kwa upande wa Sekta binafsi.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages