BWENI la
wanafunzi wasichana katika shule ya sekondari ya Moreto iliyopo tarafa
ya Msoga wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani, baada ya kuungua kwa moto na
kusababisha mali zote za wanafunzi hao kuteketea kwa moto. (Picha na
Mwamvua Mwinyi)
Na Mwamvua Mwinyi, Bagamoyo
MBUNGE wa jimbo la Chalinze, mkoani Pwani, Ridhiwani Kikwete, ametoa magodoro 50, yenye thamani ya sh.mil 2.225
kwa wanafunzi wa kike wa shule ya Sekondari Moreto, waliounguliwa na
bweni lao na kusababisha mali zote kuteketea kwa moto.
Wanafunzi
hao wapatao196, katika shule hiyo iliyopo kata ya Lugoba tarafa ya
Msoga, wilaya ya Bagamoyo, wamenusurika kifo baada ya bweni hilo
kuteketea kwa moto siku ya oktoba 5.
Moto huo umeteketeza mali zote zilizokuwemo ambazo hadi sasa hazijajulikana thamani yake.
Kufuatia kutokea kwa tukio hilo, Ridhiwani alifika shuleni hapo kutembelea na kutoa pole kwa kutokea janga hilo.
Alisema
wakumshukuru ni mungu kwani pamoja na kutokea kwa hasara ya kuteketea
kwa mali lakini hakuna madhara kwa wanafunzi yaliyotokea.
Ridhiwani aliwapa pole walimu na wanafunzi kijumla na kuwaomba wadau wengine kujitokeza kwenda kusaidia pale watakapojaaliwa.
Kwa
mujibu wa mwalimu mkuu wa shule ya sekondari Moreto, Justine Lyamuya
alielezea kuwa, tukio hilo limetokea oktoba 5,majira ya asubuhi ambapo
walianza kuona moshi mzito katika bweni mojawapo wanaloishi wasichana wa
shule hiyo.
Alisema wakati moto huo unazuka wanafunzi hao walikuwa kwenye masomo yao darasani.
"Tulifuatilia na kukuta moto umeshashika kwenye bweni hilo na jitihada za kuuzima zilishindikana"alisema mwalimu Lyamuya.
Lyamuya
alisema mali zote za wanafunzi wanaolala kwenye bweni hilo zimeteketea
kwa moto hivyo kwa sasa wanafanya tathmini kujua gharama zilizopotea.
Katika hatua nyingine jeshi la polisi mkoani Pwani linafanya uchunguzi wa tukio hilo ili kubaini chanzo cha moto.
Kamanda
wa polisi mkoani Pwani, Boniventure Mushongi, alielezea kuwa mazingira
ya jengo hilo ni yenye kutumia nishati ya solar power hivyo ni lazima
kufanya uchunguzi wa kina kujua kiini cha kuzuka kwa moto huo.
Alisema bweni hilo linakadiriwa kuwa na wanafunzi 196.
Kamanda Mushongi alisema thamani za mali za wanafunzi katika moto huo bado hazijafahamika.(P.T)
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269