Na
Magreth Magosso,Kigoma
IMEFAHAMIKA
kuwa,ubadilishwaji wa walimu katika shule za watu binafsi inachangia kwa
kushuka kwa kiwango cha elimu kwa wanafunzi husika kutokana na tatizo la walimu wanaopata ajira za muda
katika shule hizo huondoka kwa muda mfupi, hali inayowaathiri kimasomo.
Kwa
nyakati tofauti baadhi ya wanafunzi Peter Lyoba kutoka shule ya sekondari Kibogora
iliyoko wilayani Kakonko, na Lidia Shija shule ya Sekondari Bishop Mpango ya
wilayani Kibondo Mkoani Kigoma wamesema kuwa kila mwalimu ana namna ya
ufundishaji , hivyo kitendo cha ubadirishwaji wa walimu kila wakati uwapa usumbufu wa kuelewa ufundishaji wake.
``
shule binafsi wanategemea sana walimu wa muda ambao wengi ukaa muda mfupi na kuondoka kutafuta ajira
sehemu nyingine na wengine hurudi masomoni na atakayekuja anakuja na mtazamo
mpya kwa kweli inatuboa ila ndo hatuna la kubadilisha mfumo wa elimu hasa
tunaokosa nafasi shule za serikali ”walisema wanafunzi hao.
Akijibia
hilo katika mahafali ya 10 ya kuhitimu wanafunzi wa kidato cha Nne shule ya
sekondari ya Kibogora Mkuu wa kituo cha Seminary ya Iterambogo, Patrick Mahinja
alisema kuwepo kwa walimu wa kudumu au wa muda si tatizo cha msingi ni kuwapata
walimu bora wanaojua kazi na kuzingatia madili na weledi wa kufundisha
wanafunzi.
Alipohojiwa
mmoja wa walimu juu ya hilo Melesiana Leonidasi alisema sababu inayopelekea
wengi wao kuhama na kuacha kazi kwenye shule binafsi ni kutokana na kutokuthaminiwa
na waajiri hasa pale wanapopata matatizo
ya kifamilia ,hali inayopelekea kutafuata ajira serikalini ambako kuna mafao
mtambukwa , licha ya mishahara mikubwa wanayolipwa katika shule hizo.
Akitetea
hilo Makamu Mwenyekiti wa Chama cha wamiliki wa shule na vyuo binafisi (MOAF)
Jeremia Gwegenyeza alisema serika itoe uhuru wa ajira kama inavyotoa
uhuru wa maswala mengine juu ya elimu na kuongeza kuwa wengi licha ya
kufundisha wanatafuta nafasi mbalimbali serikalini kama vile uafisa elimu
uratibu nafasi ambazo hazipo katika sekta binafsi.
Alisema
wanatumia gharama kubwa kupata walimu kutoka nchi jirani kama Kenya na Uganda huku wakishawishi serikali
iliangalie hilo kwa jicho la tatu maana mtu mmoja kuja kufanya kazi hapa nchini
humgharamia kiasi cha dola 5000 na
kuwatoa hofu wanafunzi juu ya hilo.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269