Ndugu zangu,
Samwel
Sitta ( 74) na Joseph Mungai ( 73) ni marafiki wa tangu Tabora Boys.
Wawili hawa mama zao wanatoka kwenye koo kubwa za kichifu; Mama wa
Samwel Sitta, Zuena Said Fundikira, ni biinti wa Chifu Fundikira ambaye
babu yake ni Mtemi Isike Kiyungi.
Mama wa
Joseph Mungai anatokana na ukoo wa Malangalila unatokana na Chifu
Mkwawa. Hivyo, akina Malangalila na Mwamuyinga ni wajomba zake Joseph
Mungai kutoka ukoo wa Kichifu wa Mkwawa.
Hivyo,
wawili hawa mbali ya urafiki wao wa tangu shule uliowapelekea hadi
kufanya kazi kama Mawaziri kwenye Serikali za Awamu Nne, pia ni watani
wa jadi. Ni kwa vile Wahehe chini ya Chifu Mkwawa walipigana na
Wanyamwezi chini ya Mtemi Isike .
Katika
namna ya kusuluhisha mgogoro, Chifu Isike alimuozesha binti yake kwa
Chifu Mkwawa. Kikosi kidogo cha Wakonongo kilitumwa na Isike
kumsindikiza binti huyo. Walipoikaribia Iringa, Mkwawa alituma watu wake
kwenda kumpokea binti huyo nje kidogo ya Iringa mahali ambapo hadi hii
leo panaitwa Ikonongo.
Na
Wakonongo wale waliamua kuweka makazi yao hapo. Ni nje kidogo ya
Manispaa ya Iringa, na dalili za ujio wa Wakonongo hapo ni uwepo , hadi
leo, wa watu wa asili ya Kikonongo na miti mingi ya miembe waliokuja nao
Wakonongo kutoka Tabora, enzi hizo.
Ni huzuni
kwa vile marafiki hawa wawili hawakuweza kuagana. Na kwa vile, wote
wawili marafiki zao wengi ni wa wote wawili, basi, imebidi hata siku za
kuwaaga Sitta na Mungai zipishane hata kwa siku moja ili marafiki wapate
kuwaaga .
Chifu
Mungai ameagwa leo, na mwenzake Chifu Sitta ataagwa kesho. Wote wawili
watazikwa katika siku moja ya Jumamosi, mmoja Mufindi na mwingine
Urambo.
Pumzikeni Kwa Amani; Chifu Sitta na Chifu Mungai
Maggid Mjengwa.(P.T)
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269