Breaking News

Your Ad Spot

Nov 24, 2016

AMNESTY: JESHI LA NIGERIA LIMEUA WANAHARAKATI 150 WA BIAFRA

Shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limesema wanaharakati wapatao 150 wa vuguvugu linaloshinikiza kujitenga jimbo la Biafra wameuawa na jeshi la Nigeria katika kipindi cha mwaka mmoja.
Ripoti ya kurasa 60 ya Amnesty International iliyotolewa leo Alkhamisi imebainisha kuwa, maafisa usalama nchini Nigeria walitekeleza ukatili huo kwa lengo la kuzima maandamano ya wanaharakati wa Biafra, kati ya Agosti mwaka jana 2015 na Agosti mwaka huu.
Makmid Kamara, Mkurugenzi wa shirika hilo nchini Nigeria amesema wana wasi wasi kuwa yumkini idadi hiyo ikawa juu zaidi akisisitiza kuwa, vyombo vya usalama vya nchi hiyo ya magharibi mwa Afrika vilitimia nguvu kupita kiasi kuzima maandamano na mikusanyiko ya harakati hiyo.
Maandamano ya wafuasi wa harakati ya Biafra
Wakati huo huo, Sani Usman, msemaji wa jeshi la Nigeria amepuuzilia mbali ripoti hiyo ya Amnesty International na kuitaja kuwa ya upande mmoja akisisitiza kuwa, askari watano waliuawa na wanaharakati hao wakati wa maandamano ya mwezi Mei mwaka huu mbali na kushambuliwa magari ya jeshi na polisi.
Mwezi Aprili mwaka huu, polisi ya Nigeria ilidai kuwa harakati ya Biafra imehusika na mauaji ya watu 55, baada ya kugundua kaburi la umati kusini mashariki mwa nchi, madai ambayo yalikanushwa na harakati hiyo.
Nnamdi Kanu, mkuu wa Biafra
Kwa sasa polisi ya Nigeria inamzuilia Nnamdi Kanu, mkuu wa harakati hiyo inayopigania kujitenga na Nigeria eneo la Biafra la kusini mwa nchi hiyo pamoja na watuhumiwa wengine wawili wanaokabiliwa na tuhuma za usaliti na uhaini. Mwaka 1967, Kanu alitangaza uhuru wa jimbo la Biafra na kusema kuwa eneo hilo sio sehemu ya Nigeria.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages