Breaking News

Your Ad Spot

Nov 14, 2016

BAN KI MOON ALAANI KUSHAMBULIWA ASKARI WA UN NCHINI KONGO

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amelaani shambulio lililofanywa dhidi ya askari wa kulinda amani wa umoja huo huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Msemaji wa Umoja wa Mataifa jana Jumapili alielezea kusikitishwa kwake na mripuko wa bomu uliotokea Goma, katika mkoa wa Kivu Kaskazini huko kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na kuwataka viongozi wa Kinshasa kuwadhaminia ulinzi askari wa kimataifa wa kulinda amani na kuwatia mbaroni mara moja wahusika wa shambulio hilo.
Msemaji huyo wa Umoja wa Mataifa amesema, kuna wajibu wa kuitia nguvu mikakati ya jeshi la serikali ya Kongo na askari wa kulinda amani wa kimataifa ili kumaliza uasi nchini humo.
Raia wakiwemo wanawake na watoto wadogo ndio wahanga wakuu wa machafuko ya masharikimwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo

Kwa upande wake, Maman Sambo Sidikou, mkuu wa vikosi vya kulinda amani vya Umoja wa Mataifa nchini Kongo DR amesisitizia wajibu wa kushirikiana viongozi wa nchi hiyo na askari wa kimataifa katika uchunguzi wa suala hilo ili wahalifu waweze kupatikana na sheria kuchukua mkondo wake dhidi yao.
Umoja wa Mataifa umesema kuwa, msichana mmoja ameuawa na askari wawili wa kofia buluu yaani wa Umoja wa Mataifa na raia wawili wamejeruhiwa katika mripuko wa bomu uliotokea magharibi mwa mji wa Goma huko Kivu Kaskazini. Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa, askari wa kulinda amani wa kimataifa ndio waliolengwa kwenye shambulio hilo. 

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages