Nchi
zilizotia sani kwenye makubaliano ya Roma yaliyopelekea kuundwa kwa
Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) zinakutana tangu Jumatano hii.
Mkutano
hu utadumu kwa wiki moja mjini Hague, nchini Uholanzi. Huu ni mkutano
unaofanyiia kila mwaka ambao unazishirikisha nchi anachama wa Mahakama
hiyo.
Lengo la
mkutano huu ni kutathmini shughuli za Mahakama na kuidhinisha bajeti
yake. Lakini mwaka huu mkutano huu unafanyika katika mazingira tete
tangu nchi tatu za Afrika9 Burundi, Afrika Kusini na Gambia) kutangaza
nia yao ya kujiondoa katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC).
Wakati wa
mkutano wa nchi wanachama, Mwendesha Mashitaka wa ICC, Fatou Bensouda
amesema kuwa baadhi ya viongozi wa nchi za Afrika hawataki wanyooshewe
kidole kwa makosa wanayotekeleza, huku wakipinga Mahakama ya Kimataifa
ya Uhalifu (ICC) ili wasiweze kufuatilia.
Hata
hivyo amesema kusikitishwa na uamuzi wa kujiondoa kwa baadhi ya nchi za
Afrika katika makubaliano ya Roma yaliyopelekea kuundwa kwa mahakama
hiyo. Kwa mujibu wa Fatou Bensouda uamuzi wa viongozi hao unaitenga
dunia katika ulimwengu wenye sheria, kwenye lengo la sheria kwa wote.
Bila
shaka, Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu imeendelea kuwa na wasiwasi
tangu kukosolewa na nchi kadhaa kutoka afrika ambazo zinaituhumu kwamba
uamuzi wake huchukuliwa kutoka kwa nchi za magharibi.
Hayo
yanajiri wakati Mahakam hio iliituhumu Marekani Jumanne wiki hii kwamba
ilitekeleza uhalifu wa kivita nchini Afghanistan. "Msiondoke" Mwenyekiti
wa Baraza la nchi wanachama wa Mahakam ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC),
Waziri wa Sheria wa Senegal, alituma ujumbe kwa nchi hizi tatu:
akizitaka 'kutojiondoa'. "Tumesikia madai yenu, ni halali.
Ni lazima
tutafutiye ufumbuzi mgogoro huu. " Kwa upande wake, Kamishna wa Umoja
wa Mataifa wa Haki za Binadamu Zeid Ra'ad al-Hussein alizungumzia
masikitiko yake, lakini akasema kujiondoa kwa nchi hizi ni njia tu ya
kulinda viongozi wa nchi hizo dhidi kufunguliwa mashitaka.
Amesisitiza
hasa nchi kadhaa za Afrika miongoni mwa 34 ambazo zingependa kuendelea
kuwa wanachama wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC).RFI
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269