Inspekta wa Polisi katika mkoa wa Ituri
nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ameripoti kutiwa mbaroni kundi
moja la watu wenye silaha katika mji wa Bunia nchini humo.
Joseph Alimasi Inspekta wa Polisi katika mkoa wa Ituri
ametangaza kuwa kundi hilo lililokamatwa la watu 20 limepelekea
kuhitimishwa mauaji katika mji wa Bunia makao makuu ya mkoa wa Ituri.
Alimasi ameongeza kuwa askari usalama juzi Jumanne waliwaarifisha watu
hao kwa Jefferson Abdallah Penembaka Gavana wa mkoa wa Ituri. Inspekta
wa polisi wa mkoa wa Ituri amepongeza hatua hiyo ya askari usalama wa
huko Bunia na kuwatolea wito wakazi wa mji huo kuendeleza ushirikiano
kati yao na polisi.
Hii ni katika hali ambayo baadhi ya wakuu wa taasisi za kiraia huko
Kongo wamesema wana wasiwasi na kuwepo makundi ya watu wenye silaha
katika mji wa Bunia. Maeneo ya mashariki na kaskazini mwa Jamhuri ya
Kidemokrasia ya Kongo yanakabiliwa na ukosefu wa amani kwa miaka 20
sasa.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269