Breaking News

Your Ad Spot

Dec 9, 2016

DENMARK YATOA SH.MILION 47,KAKONKO MKOANI KIGOMA

 NA MAGRETH MAGOSSO,KIGOMA 

 NCHI ya Denmark imesaidia kiasi cha Cha fedha cha Sh,milioni 47,zimetumika katika ujenzi wa mradi wa Jengo la wafanyabiashara mbalimbali wa wilaya ya Kakonko mkoani humu,uliolenga kutoa huduma za kitaalamu juu ya biashara na namna ya kupata soko za bidhaa hizo. Akithibitisha hilo Ofisa Biashara wa wilaya ya kakonko Erasmus Kishongoli katika ukabidhiwaji wa jengo hilo kwa Mkurugenzi mtendaji wa wilaya hiyo Lusubilo Joel Kanal alisema kwa msaada wan chi hiyo kupitia shirika la Maendeleo ya biashara la( LIK) wamefanikiwa kujenga jengo hilo,kwa kiasi hicho cha fedha,ambapo itawapatia uelewa wafanyabishara juu ya shughuli zao hasa upatikanaji wa soko kwa bidhaa zenye kiwango cha kimataifa. Akipokea jengo hilo Mkurugenzi wa wilaya hiyo Lusubiro Joel alisema kukamilika kwa jengo hilo ni fursa kwa wafanyabishara kupunguza gharama za kufuata huduma za ushauri wa kibiashara mjini na wawatumie wataalamu ili kuongeza ufanisi wa bidhaa zao na kukidhi soko kwa walaji. Akitoa mwito kwa wafanyabishara Mkuu wa wilaya hiyo Kanali Hosea Ndagala alisema kuwa lengo la Kituo hicho ni walengwa kufanya shuguli zao kitaalamu na usasa na kuwasihi walitumie ipasavyo mara litakapoanza shuguli zake na watumie fursa ya ujirani mwema na wakazi waishio mpaka mwa Nchi Jirani ya Burundi ,ili kubadilishana uzoefu. ‘’Itabidi mtumie nafasi hii kufanyabiashara na majirani zenu kwa kuutumia vizuri mpaka huu, ikiwa ni pamoja na kupata elimu ya biashara kwakuwa kituo hik kitakuwa na mambo yote muhimu lakini hata watoa huduma watatakiwa kuacha urasimu ambao uchangia kukwamisha wengi kusonga mbele alisema Kanali Ndagala’’ Kwa upanmde wa wafanyabiashara Musa Marko na Hamisa Amad kwa nyakati tofauti walisema changamoto ya elimu ya ujasiliamali ni moja ya janga la kutolipa kodi,kwa kuwa wengi hawajui kiwango cha ulipaji kodi kulingana na biashara hali inayochangia kufanya bishara zao gizani. Kituo hicho kinatarajia kutoa huduma za uhamiaji usajili wa majina ya Biashara Elimu ya ulipaji Kodi na kuwaunganisha wafanyabiashara na Taasisi za serikali na litakuwa likitumia mfumo wa kisasa wa kielectronic ili kurahisishahupatikanaji wa huduma . Mwisho.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages