NA MAGRETH MAGOSSO, KIGOMA
MTU Mmoja jina lake (hifadhini ) atafikishwa
mahakama ya wilaya ya Kigoma kwa tuhuma
za kukutwa na Brifkesi ikiwa na risasi 408 za bunduki aina ya SMG na SAR.
Akithibitisha Kauli hiyo juzi
ofisini kwake kigoma ujiji, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma Ferdinand Mtui
alisema Desemba,5 ,2016, saa 2.20 katika kijiji cha Makere, tarafa ya makere
wilayani kasulu askari polisi wakiwa katika doria walipewa tarifa na wananchi
wema juu ya mtuhumiwa huyo na ndipo wakamtia nguvuni.
“walimfikisha katika kituo cha
polisi makere, walimpekua hiyo brifikesi na kukuta risasi sanjari na nguo, vitau kukamatwa kwake ni uthubutu wa wananchi wachache kulisaidia jeshi
la polisi katika kupambana na wahalifu ambao wanakiuka maadili ya taifa kwa
ujumla” alifafanua Kamanda huyo.
katika tukio la pili Mwanamume
mmoja aliyefahamika kwa majina ya Hussein Athuman (36) mkazi wa mwanga vamia
mtaa wa Msikiti madina Manispaa ya Kigoma Ujiji wilaya ya kigoma mkoani
humu, amejinyonga kwa kutumia kamba ya katani baada ya kukimbiwa na mkewe.
Akifafanu hilo Kamanda Mtui alisema
Desemba,6 ,mwaka huu saa 4.00 asubuhi kaka wa marehemu Salum Hamimu alienda
kumtembelea ndugu yake huyo baada ya kuelezwa na dada yao aishie mkoani Tabora
kuwa usiku wa desemba,5 mwaka huu marehemu alimpigia simu dada huyo kuwa mkewe
kaondoka nyumbani .
Alisema ana siku ya Nne haonekani nyumbani na kukiri walikuwa na ugomvi, hivyo amweleze
kakake kuwa atachukua mamuzi magumu ,ndipo siku iliyofuta kakake alienda
nyumbani kwa mlengwa na alipogonga alikuta ukimya mkubwa alipotumia nguvu na
kufungua mlango ndipo alikuta nduguye amejitundika darini kwa kamba ya katani.
Aidha katika msako wa wahalifu
walifanikiwa kukamata wahamiaji haramu 63, pombe ya moshi lita 224 na bhange
debe 02,bila kutoa ufafanuzi wa wahalifu hao na vithibitisho hivyo pia litoa
rai kwa wananchi kuwa kila mwananchi anajukumu la kutii sheria bila
shuruti kutoa tarifa kwa vyombo vya usalama kwa mtu yeyote mwenye kiashiria cha
uhalifu ili sheria ichukue mkondo wake.
mwisho.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269