Serikali
ya rais Barack Obama imefutilia mbali mkataba wa kuiuzia Saudi Arabia
baadhi ya silaha. Hatua hiyo ni ishara ya kupinga kampeni ya mshirika
wake huyo nchini Yemen ambayo imesababisha mauaji ya raia wengi.
Utawala
wa Rais Barack Obama umeamua kutowauzia baadhi ya silaha Saudi Arabia
ambayo ni moja kati ya nchi washirika wa Marekani. Kwa mujibu wa afisa
mmoja wa cheo cha juu mjini Washington, ushirikiano wa masuala ya
usalama sio kitu cha mchezo na kwamba Marekani imeamua kutokuendelea na
uuzaji wa vifaa vya kijeshi kwa Saudi Arabia kutokana na taifa hilo
kubwa kutoridhika na jinsi Saudi Arabia inavyoendelea kufanya makosa
katika operesheni yake ya anga nchini Yemen.
Wakati
huo huo miili 11 ya watu imepatikana imetupwa katika hifadhi. Miili hiyo
ya wanaume ambayo ilikuwa haina vichwa imepatikana imetupwa katika
hifadhi ya al-Hiswa iliyopo magharibi ya mji wa Aden. Ingawa taarifa
kamili kuhusiana na mauaji hayo bado hazijatolewa lakini gazeti la Aden
la al-Ghad limeripoti kwamba miili hiyo ilitupwa mahala hapo kwa zaidi
ya mwezi mmoja.
Mji wa
Aden wa pili kwa ukubwa nchini Yemen umekumbwa na visa vya uvunjaji
sheria wakati ambapo makundi yaliyojihami kwa silaha kama kundi
linalojiita dola la Kiislamu IS na kundi la kigaidi la al Qaeda
yanaendelea kuwa na nguvu katika kipindi chote cha mwaka mmoja na nusu
baada ya wafuasi wa Rais Abd-Rabbu Mansour Hadi kulifurusha kundi la
Houthi lililokuwa linaungwa mkono na majeshi ya ushirika wa nchi za
kiarabu. Takriban watu elfu 10 wameuwawa katika machafuko hayo
yaliyodumu kwa miezi 20 na ambayo yamesababisha hali mbaya ya kibinadamu
katika nchi hiyo masikini.
Juu ya
watu wanne waliouwawa katika mashambulizi ya hivi karibuni nchini Yemen,
watu watatu walikuwa watuhumiwa wa kundi la kigaidi la Al Qaeda na
mmoja alikuwa ni kamanda wote waliuwawa baada ya gari walilokuwemo
kushambuliwa na ndege isiyo na rubani mashariki ya mji mkuu wa Sanaa.
Inaaminika kuwa ndege hiyo isiyo na rubani ilikuwa ya Kimarekani.
Marekani
imethibitisha kutumia ndege zake hizo zisizo na rubani katika mapambano
dhidi ya makundi ya wapiganaji wa Kiislamu wenye msimamo mkali nchini
Yemen lakini imekuwa haisemi pale ndege zake hizo zinapotumiwa kufanya
mashambulio.DW
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269