Breaking News

Your Ad Spot

Dec 29, 2016

WFP: HUENDA TUKASITA KUPELEKA MISAADA JAMHURI YA AFRIKA YA KATI

Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) limeonya kuwa kama litaendelea kukabiliwa na matatizo litalazimika kusimamisha upelekaji misaada kwa maelfu ya wakimbizi nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati.
WFP limezitaka nchi na mashirika yanayotoa misaada kuongeza misaada yao ya kibinadamu kwa shirika hilo ili ufikishaji misaada na huduma muhimu za maisha kwa wakimbizi wanaokabiliwa na hali mbaya nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati iweze kuendelea.
Uhaba wa fedha katika mwaka huu unaomalizika wa 2016 umeathiri sana shughuli za ufikishaji misaada na utoaji huduma za kibinadamu wa Shirika la Mpango wa Chakula Duniani; na ndiyo maana ni watu wapatao laki nne tu kati ya wakimbizi milioni moja wanaohitaji misaada ya kibinadamu katika Jamhuri ya Afrika ya Kati wameweza kupatiwa misaada na shirika hilo.
Wakimbizi wa Jamhuri ya Afrika ya Kati walioko Cameroon
Tangu mwaka 2013 kufuatia kupinduliwa utawala wa rais wa wakati huo Francois Bozize na wanamgambo wa kundi la Seleka, Jamhuri ya Afrika ya Kati imekuwa ikishuhudia machafuko, mapigano na vita vya ndani.
Mapigano na mashambulio dhidi ya raia yamekuwa sababu ya kuvurugika amani, kuuawa, kujeruhiwa na kubaki bila ya makaazi zaidi ya robo moja ya raia milioni nne na laki nane wa nchi hiyo.
Rais Faustin-Archange Touadéra wa Jamhuri ya Afrika ya Kati
Hata hivyo tangu Rais Faustin-Archange Touadéra aingie madarakani mwezi Machi mwaka kufuatia uchaguzi wa kidemokrasia, kiongozi huyo amekuwa akisisitizia udharura wa kurejeshwa amani na usalama nchini humo.../

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages