Breaking News

Your Ad Spot

Feb 16, 2017

MATTIS: UJUMBE WA KUGAWANA GHARAMA UMEPOKELEWA VIZURI

Mwito wa Marekani kwa wanachama wa jumuiya ya kujihami ya NATO kuongeza matumizi yao ya ulinzi ulitarajiwa na umepokelewa vizuri, waziri wa ulinzi wa Marekani James Mattis alisema leo baada ya kuhudhuria mkutano wake wa kwanza na mawaziri wa ulinzi wa NATO mjini Brussels. Jana Mattis aliwaambia mawaziri wenzake wa NATO kwamba Marekani itapunguza ushiriki wake kwa muungano huo hadi pale mataifa wanachama yatakapofanya mipango kufikia kiwango kinachotakiwa na NATO cha matumizi ya ulinzi cha asilimia 2 ya pato jumla la taifa. Siku ya Jumatano Mattis aliwaambia wanachama wa NATO kwamba wanapaswa kutayarisha mpango hadi ifikapo mwishoni mwa mwaka huu juu ya njia za kufikia kiwango hicho cha asilimia 2, ambacho kiliwekwa mwaka 2014 kwa mujibu wa mabadiliko ya hali ya usalama wa dunia. Muda wa mwisho kufikia lengo hilo ni mwaka 2024.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages