Breaking News

Your Ad Spot

Mar 8, 2018

MWENYEKITI WA UWT GAUDENTIA KABAKA ATEMBELEA HOSPITALI YA MBAGALA KUADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI, LEO

 Mwenyekiti wa Umoja wa wanawake Tanzania (UWT) Gaudentia Kabaka akifurahia mtoto wa kike, alipotembelea wodi ya Wazazi katika Hospitali ya Mbaala Rangi tatu, wilayani Temeke Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Siku ya Mwanamke Duniani, leo Machi 8, 2018. Mapema Mama Kabaka akiambatana na kina mama mbalimbali wakiwemo viongozi wa UWT kutoka maeneo mbalimbali, alishiriki kufanya usafi na baadaye kutoa zawadi mbalimbali kwa uongozi na waonjwa kwenye Hospitali hiyo. Kulia ni Mariam Salum, mzazi wa mtoto huyo. 
 "Haya Mama chukua kichana chetu.." akasema Mama Kabaka wakati akirejesha mtoto kwa Mariamu Salum baada ya kumkabidhi zawadi ya kanga.
 Mama Gaudentia Kabaka akitoa zawadi za juisi kwa kina mama waliojifungua katika hospitali hiyo ya Mbagala Ranitatu
 Baadhi ya Kinamama wakaiwa na zawadi za kanga na sabuni ambazo Mama Kabaka aliawa kwa kina amama waliojifunua katika hospitali hiyo.
 "Hebu chukua kanga hii kutoka kwa kina mama wenzako.." akasema Mama Kabaka wakati akimkabidhi Mwajuma Ally aliyejfungua mtoto katika hospitali ya Mbagala Rangitatu
 "Loooh mtoto umejifunugua mtoto mzuri sana..." akasema Mama Kabaka 
 Kisha akampatia zawadi ya mche wa sabuni
 Diwani wa Viti Maalum CCM, Mariam Mtemvu na wenzake wakimsalimia mmoja wa Kina mama aliyekuwa katika Wodi ya Wazazi baada ya kujifungua katika hospitali ya Mbagala Ranitatu, leo
 Ofisa wa Makao Makuu ya UWT Ndugu Kisa wapili kulia, akiwa na kina mama weningine.
 Ofisa wa Makao Makuu ya UWT Ndugu Kisa (kushoto), akiwa na wauguzi na kina mama weningine kwenye hospitali hiyo ya Mbagala Ranitatu leo. 
 Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Gaudentia Kabaka akimpa zawadi ya kanga mmoja wa wauuzi katika hospitali ya Mbagala Rangitatu wakati wa ziara hiyo
 "Wauuzi na Madaktari honereni kwa kazi nzuri na hasa kwa kujali afya za kina mama na watoto...endeleni kuchapa kazi tupo pamoja nanyi", alisema Mama Kabaka wakati akizunumza na baadhi ya wauguzi na madaktari wa hospitali ya Mbagala Ranitatu wakati wa ziara hiyo. Kushoto ni Matroni wa wodi ya Wazazi Maria Lumambo
 Mama Kabaka akiendelea kuzunumza nao
 Mweneyekiti wa UWT Gaudentia Kabaka akifuatana na Matroni wa Wodi ya Wazazi Maria Lumambo, baada ya kutoka wodini kuwaona na kuwapa zawadi wazazi
 Mweneyekiti wa UWT Gaudentia Kabaka akizungumza baada ya kutoka wodini kuwaona na kuwapa zawadi wazazi
 Picha ya kumbukumbu
Mweneyekiti wa UWT Gaudentia Kabaka akiwa tayari kuondoka kwenye Hospitali ya Mbagala Rani tatu baada ya ziara yake leo. PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages