Breaking News

Your Ad Spot

Jun 15, 2014

MAMA MZAZI WA KIM KARDASHIAN NUSURA AVUNJE NDOA YA KANYE WEST, KISA???

Khloe, Kris Jenner, Kanye West na Kim Kardashian
Khloe, Kris Jenner, Kanye West na Kim Kardashian
Kadri siku zinavyozidi kwenda, ndivyo teknolojia inavyozidi kushika kasi hiyo ni kufati  wezi wa mitandaoni maarufu kama Hackers kumfanyia kitu mbaya mwanafamilia wa  Keeping Up With Kardashian  ‘Kris Jenner’  kwa kuihack akaunti yake ya  mtandao wa Instagram yenye wafuasi zaidi ya milioni 3  na kisha kuandika ujumbe  uliotafsiriwa kuwa ni wa uchonganishi dhidi ya wakwe zake.
Moja ya ujumbe ulisomeka ”Simpendi Kanye West! Najifanyisha kwa maslahi ya binti yangu”  haikupita muda ukawekwa ujumbe mwingine uliokuwa ukimlenga French Montana ”Yeye sio Mweusi, kama ningelkuwa nawafagilia watu weusi ningetembea nae mmoja”. Hata hivyo ujumbe huo ulifutwa haraka.
Kris Jenner ni mama mzazi wa Kim na khloe ambao wote wapo kwenye mahusiano ya kimapenzi na wakali hao wa muziki wa Hip Hop waliohusishwa kwenye sakata hilo  huku Kim akiwa ni mke halali wa ndoa wa Rapa Kanye aliyezaa nae mtoto mmoja wa kike NorthWest wakati Khloe yupo kwenye mahusiano ya siri na French Montana.
Kris Jenner
Pichani ni Ujumbe uliotaka kuvunja ndoa ya Kim na Kanye

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages